Home » » MBUNGE AWATAKA KINAMAMA WAJAWAZITO KUJENGA TABIA YA KUPIMA AFYA ZAO, ALANAO CHAKULA CHA KRISMAS NDANI YA WODI YA WAZAZI

MBUNGE AWATAKA KINAMAMA WAJAWAZITO KUJENGA TABIA YA KUPIMA AFYA ZAO, ALANAO CHAKULA CHA KRISMAS NDANI YA WODI YA WAZAZI

na Walter Mguluchuma
Mpanda

Akina mama  wajawazito wa Mkoa wa Katavi  wametakiwa  kuachana na tabia  ya  kuchelewa  kwenda  hospitalini na kwenye  vituo  vya afya  kupima afya  pindi wanapo kuwa  wamepata ujauzito  ili  kuepuka  vifo vya mama na mtoto.

ushauri huo   ulitolewa hapo juzi na mbunge wa viti maalumu  mkoa wa katavi  Dr  Pudensiana kikwembe  alipo  kuwa  akizungumza na akina mama wajawazito  kwenye  wodi ya wazazi    katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda alipo  kuwa  akiwafariji   wakati wa maadhimisho ya  sikukuu ya krismasi.

Dr Kikwembe (CCM) mbali ya kuwafariji  wakinana wajawazito  pia  aliwapatia  vitenge  kwa akina mama wote  45 walio kuwa wamelazwa ndani ya wodi hiyo  pia alitowa chakula kwa wagonjwa wote  na vinywaji  baridi  katika wodi   zote  sita  za hospitali  hiyo ya wilaya ya Mpanda.

 Mbunge huyo alisema   ni vizuri watu  wakapatiwa elimu   ya afya  ili kuepukana na tatizo sungu  lililopo Mkoani Katavi   la kuwachelewesha wagonjwa walio  wengi wanao   kuwa wagonjwa  wanapelekwa hospitalini  wakiwa wameshoka   kutokana na kutopelekwa mapema Hospitalini.

 Alifafanua  kuwa madakitari wamekuwa wakipewa lawama ambazo sio  zao    ili kuokoa uhai   watu  wawe na tabia ya  kutibiwa mapema  na sio  kukimbilia kwanza kwa waganga wa kienyeji ambao   sio  wataalumu  wa  kuweza kutambua magonjwa mbambali.

 Dr Kikwembe aliwashauri akinana  mama wajawazito  na wazazi  kwa kufuata mashariti ya   afya  kwa kutumia vyandarua  ili kuepukana na vifo vinavyo sababishwa na ugonjwa wa maralia  na pia kumuunga mkono mama  Salima Kikwete  kwenye jihihada zake za  kupambana na ugonjwa wa maralia.

 Alisema  wapo  baadhi ya watu   wamekuwa wakipewa msaada wa vya ndarua na wao  wamukuwa wakivitumia kwa matumizi mengine  ya  kuvulia  samaki na  kufungia kuku  hivyo  amewataka waachane na tabia hiyo.

Pia aliwashauri wakinamama wajawazito wawashirikishe waume zao pindi wanapo kuwa wanaenda cliniki ili na wao wanaume waweze kuwa wakijua maendeleo ya afya zao tofauti na ilivyo sasa ambavyo inaonekana swala la cliniki linamhusu mama mjamzito peke yake.

 Dr Kikwembe   aliwaomba madakitari na wauguzi  waendelee na moyo  wa kufanya kazi   licha  ya upungufu   uliopo  wa watumishi wa idara ya afya  kwani serikali inalitambua hilo  na ndio maana  ina mpango wa kuongeza vyuo  yva madakitari  na wauguzi

Kwa  upande wake  muuguzi mkuu wa hospitali hiyo   Evelina Wampembe alimshukuru  Mbunge huyo wa viti maalumu na amewaomba    viongozi wengine waige mfano wake

 Pia  wampembe  alisema kuwa hospitali  hiyo  inakabilwa na changamoto mbalimbali  ikiewepo ya  upungufu wa watumishi wa affa  ambapo  waliopo ni 50 wakati mahitaji  ni watumishi  150
Changamoto  nyingine aliitaja kuwa  ni miundo  mbinu mibovu ya vyoo vya nje  ambavyo  ni vyakizamani vya matundu ya chuo  ambapo  husababisha baadhi ya kuna mama wanapo jifungua kutupia mtoto  kwa makusudi.

Muuguzi huyo wa Hospitali alieleza kuwa katika skukuu ya krismasi jumla ya watoto 13 walizaliwa katika wodi hiyo ambapo watoto kumi walikuwa ni wakiume na tatu walikuwa ni wakike.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa