Home » » SHEIKH ANUSURIKA KICHAPO KUTOKA KWA WAUMI WA KIKRISTU.

SHEIKH ANUSURIKA KICHAPO KUTOKA KWA WAUMI WA KIKRISTU.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

  
Na   Walter  Mguluchuma .
        Katavi.



SHEIKH  Hamisi Kikoti amenusurika kichapo kutoka kwa waumini wa
kikristo baada ya kutoa kauli ya maudhi dhidi yao wakati wa maziko ya
askari mgambo   maarufu na   aliyekuwa   akiaminika na  wananchi wa  Kata  nzima, Tano Nkuba .

Tafrani hiyo ilitokea  hivi karibuni  katika eneo la makuburi katika
kijiji cha Majalila kilichopo katika wilaya ya Tanganyika katika mkoa
wa Katavi  ambapo waumini wa  kikristo walisusa maziko ya askari
mgambo huyo na kuamua kurejea msibani

Hata hivyo Diwani wa Kata ya Ntongwe kilichopo kijiji hicho cha
majalila , Frank Kibigazi alifanikiwa kuumaliza mgogoro huo  baina ya
waumini wa madhehebu  hayo mawili  kufikia uamuzi wa kutoshirikiana
kwa lolote lile  kijijini humo .

Akifafanua diwani huyo alieleza kuwa baada ya kuibuka kwa mgogoro huo
baina ya waumuni wa kikristo na wenzao wa kiisilamu aliwakutanisha
viongozi wao ambapo walikubalina kuwa wakikutana na waumini waokwenye
nyumba zao za ibada watawatangazia kuwa mgogoro huo umekwisha .

Mgogoro huo ulisababishwa na Sheikh Kikoti wakati alipokuwa akiongoza
ibada ya maziko ya askari mgambo wa kijiji hicho ambapo alitoa  kauli
ambazo waumini wa kikristo walidai  kuwa amewakashifu  na kusababisha
vurugu  kuibuka  makaburini huku wakiristu  wakitaka  kumpiga.
.
Sheikh  huyo   anadaiwa  kutowa  kauli kuwa   waislamu  ndugu zao ni  waislamu  na  hivyo  wasali  sana   wasiwe     kama   wenye   majina ya  John  ambao  hawajuwi kusali na wanaabudu ovyo ovyo.
Diwani  huyo   alieleza  kuwa  mgogoro  huo   alifanikiwa kuumaliza  kwa  kushirikiana  pia  na    baadhi ya  wazee   wa   Kijiji   hicho.

Mwalimu wa Dini wa Kanisa katoliki kijijini humo , Credo Lusambo

aliingilia kati na kuwasihii waumuni wake wapunguze jazba  lakini hata

walipomwomba Sheikh Kikoti  kuwaomba radhi alikataa mpaka diwani

Kibigazi alipoingilia kati na kuwakutanisha viongozi wa dini wa pande

hizo mbili .



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa