Home » » HOT NEWS: WAGANGA WA TIBA ZA ASILI WATAKIWA KUACHA TABIA YA KUFANYA NGONO NA WANAWAKE WENYE MATATIZO YA UZAZI.

HOT NEWS: WAGANGA WA TIBA ZA ASILI WATAKIWA KUACHA TABIA YA KUFANYA NGONO NA WANAWAKE WENYE MATATIZO YA UZAZI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na   Walter  Mguluchuma.
    Katavi

WAGANGA wa kiume  wa tiba asili  na tiba mbadala  mkoani Katavi
wametakiwa  kuacha  mara moja tabia   ya kufanya ngono  na  wanawake
wenye matatizo ya uzazi ambao hawajabahatika kupata watoto   ili
waweze kupata ujauzito na  kujifungua salama .



Rai hiyo ilitolewa  jana  na Mkurugenzi wa Tiba ya Asili  kutoka
Wizara  ya Afya , Maendeleo  ya Jamii , Jinsia , Wazee  na Watoto , Dk
Paul Mhume wakati alipokuwa akifungua mafunzo ya siku moja
yaliyowashirikisha  waganga wa  tiba asili  na tiba mbadala kutoka
Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi .

Mafunzo hayo yalifunguliwa na na Katibu Tawala wa mkoa wa Katavi ,
Kamishina   wa Polisi , Paulo Chagonja .

“ Wanawake  ambao  hawajabahatika kupata  watoto  kutokana na matatizo
ya uzazi  wamekuwa wakikimbilia kwa  waganga  wa tiba ya asili  kwa  kuwa wanawaamini sana.…


wamekuwa  wakiambiwa  na waganga hao kuwa  ili  waweze kupata watoto
lazima  wafanye  nao  ngono  tena  bila kutumia kinga  hii
inahatarisha afya za wanawake hao  kwani wanaweza kupata  maambulizi
ya magonjwa yanayosababishwa na ngono  zembe “ alieleza .

Aliongeza kuwa visa hivyo  vinavyovyanywa na waganga hao  kwa wateja
wao wa kike  vimekuwa vikisababisha  wanawake  hao  kupewa ujauzito na
 waganga hao   bila waume zao kufahamu .


Aliwatahadharisha waganga hao kuwa kwa kufanya hivyo wanajivunjia
heshima  mbele ya jamii  inayowazunguka .

Kwa upande  wake Msajili wa Baraza  la Tisa Asili na Tiba mbadala , Dk
Ruth Suza alisema kuwa  baadhi  ya waganga  wa tiba asili na tiba
mbadala  wamekuwa wakiwadanganya  wateja wao  kuwa ili watajirike
lazima  kwanza  wawabake  binti zao  wadogo  kiendo ambacho ni kosa la
jinai .



“Lazima mzingitie  miiko na maadili ya kazi yenu  kwani wapo  miongoni
mwenu wanaosababisha uvunjifu wa amani  kwa  kupiga ramli chonganishi
aghalabu  husababisha mauaji “ alisisitiza


Aliwaonya waache tabia  ya kuwaweka  akina  wajawazito  nyumbani kwao
wakati ambapo hawawezi  kuwazalisha badala yake watoe  taarifa  kwenye
vituo  vinavyotoa huduma za afya ili waweze  kupatia tiba sahihi  na
kuepusha vifo vya wajawazito na watoto  visivyo vya lazima .


Kwa  upande wake Katibu  Tawala  wa  Mkoa  wa  KataviChagonja
aliwataka  waganga hao  wazingatie  maadili   kwa kuacha kupiga
ramli chonganishi  pindi wanapokuwa wanawahudumia wateja wao .


Mganga  Mkuu wa  Mkoa wa  Katavi ,  Dk   Yahaya  Hussein  alisema
mkoa huo unaendelea na zoezi  la kusajiri   waganga  wa tiba  asili
tiba  mbadala  kupitia  waratibu  wa  ngazi ya  wilaya  kwa
kushirikiana  na uongozi  wa waganga   wa tiba  asili .


Alisisitiza kuwa lengo la zoezi hilo ni kuhakikisha   waganga  wote
wa tiba asili na tiba mbadala   wanafanya kazi zao  kwa kufuata
kanuni  na taratibu za  Serikali
 Alisema kuwa  hadi sasa   Mkoa wa  Katavi unao waganga wa Tiba asili na tiba mbadala 316  ambao wanaotambulika  na  165 wakiwa  tayari wameisha  sajiriwa .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa