Home » » WANAFUNZI WASOMEA CHINI YA MWEMBE KUTOKA NA UPUNGUFU WA MADARASA.

WANAFUNZI WASOMEA CHINI YA MWEMBE KUTOKA NA UPUNGUFU WA MADARASA.


  Na  Walter   Mguluchuma .
           Katavi .
Wanafunzi wa Shule ya  Msingi  Kafisha  Tarafa ya  Karema  Wilaya ya  Tanganyika   Mkoa wa  Katavi   wanalazimika kusomea  masomo yao  huku wakiwa  chini ya miti ya miembe kutokana  na  shule  hiyo  yenye mikondo saba  kuwa na madarasa  mawili tuu ya kusomea .
  Hayo  yalielezwa  hapo  juzi  na    Diwani wa  Kata ya  Ikola  Philimoni  Moro wakati  alikuwa  akizungumza  mbele ya Wandishi wa  Habari kuhusiana  na   changamoto  zinazoikabili  Kata  hiyo iliyoko  mwambao mwa  Ziwa  Tanganyika .
 Alisema   Shule  hiyo ya  Msingi  Kafisha  inajumla ya Wanafunzi zaidi ya  600 na  inavyumba  viwili tuu  vya  madarasa  huku  ikiwa na  mikondo ya kuanzia   darasa la kwanza  hadi  la  saba  na ina Walimu  saba
Kutokana  na  uhaba  huo   mkubwa wa  vyumba  vya   madarasa  wanafunzi wa   shule  hiyo    wanalazimika  kusomea   chini ya   miembe   huku  wengine  wakiwa  wanapigwa na jua .
 Diwani   Moro   alisema  kipindi cha   mvua  za  masika  kimekalibia  kuanza   hivyo   yeye   kama   Diwani wa  Kata   hiyo   hajui  wanafunzi wa   shule  hiyo watakuwa  wanasomea wapi wakati  mvua  itakapokuwa  inanyesha.
 Alieleza  pamoja  na  jitihada  zilizofanywa  na  Wananchi  za  kuchangia   madawati   katika   shule  hiyo ya   Kafisha   wananchi   wanaweza  wakavunjika  moyo   baada ya  kuona   madawati waliochangia  yakiwa yako nje yanapingwa tuu na jua .
Nae  Mbunge wa  Jimbo  hilo la  Mpanda  Vijijini  Moshi  Kakoso alikiri  kuwepo   kwa  tatizo la  upungufu  mkubwa  wa  vyumba  vya   madarasa
Alisema  tatizo hilo    kwenye  jimbo hilo    ni  la muda  mrefu na  ndio  maana    miaka   mine  iliyopita  yeye  kama   Mbunge  aliweza  kutowa  msaada wa   madawati  kwenye  baadhi ya  shule  ambazo wanafunzi walikuwa wakisomea  chini  na pia  alichangia  vifaa vya ujenzi wa  majengo ya  madarasa .
  Hivyo  aliwaomba   Madiwani  kufanya  kazi ya kuwaelimisha  wananchi juu ya  umuhimu wa  kuchangia  uenzi wa  madarasa,nyumba za  Walimu  na   matundu  ya vyoo.

MWISHO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa