Home » » AGIZO LA DC MPANDA LAANZA KUTEKELEZWA

AGIZO LA DC MPANDA LAANZA KUTEKELEZWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Agizo alilolitowa na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi Paza Mwamlima la kupiga marufuku biashara ya kuuza pomba na kucheza polu  na kucheza bao wakati wa kazi limeanza kutelelezwa katika Manispaa ya Mpanda  .
Mkuu wa Wilaya hiyo hivi karibuni alitowa agizo la kupiga marufuku uuzaji wa pombe za iana   zote  katika muda wa kazi katika maeneo yote ya Wilaya ya Mpanda.
Mwamlima  mbali ya agizo hilo la kuuza pombe pia alipiga marufuku watu kucheza  polu na  bao pamoja na watu kuacha kukaa kwenye vijiwe vikiwemo vijiwe vya kawahawa wakati wa muda wa kufanya kazi.
Kufuatia agizo hilo la DC wa Mpanda  wafanyabiashara wanao miliki bar  na grosali mbalimbali katika manispaa ya Mpanda  wametii agizo hilo kwa  kuacha kuuza vinywaji vikari muda wa kazi .
Mmoja wa wafanyabiashara  mmiliki  wa Bar maarufu  ya Deluex katika Manispaa hiyo alisema  ameanza kuteleleza agizo hilo la Mkuu wa Wilaya kwa kusitisha kuuza vinywaji vikari muda wa kazi .
 Alisema  huduma ya vinywaji vikari vinaanza kutolewa  kwenye bar yake kuanzia saa tisa na nusu ikiwa ni kutekeleza agizo lililotplewa na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda .
Miongoni mwa maeneo ambayo yalikuwa yameshamiri uuzaji wa pombe muda wa kazi  katika Manipaa ya Mpanda ni mtaa wa Fisi na  Mtaa wa Simba  ambapo wamiliki wa Grosali  na bar katika mitaa hiyo wametii agizo hilo .
Na pia kwenye yale maeneo ambayo watu walikuwa wakishinda wanacheza polu sasa hivi mchezo huo wanaanza kucheza saa kumi jioni ikiwa ni katika kuteleza agizo hilo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa