Home » » MWENYEKI WA CHADEMA WA MKOA WA KATAVI APEWA ONYO KWA KUWA NA MAKUNDI NDANI YA CHAMA

MWENYEKI WA CHADEMA WA MKOA WA KATAVI APEWA ONYO KWA KUWA NA MAKUNDI NDANI YA CHAMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter Mguluchuma
  Katavi
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo  CHADEMA wa Mkoa wa Katavi Laulenti Mangeshi  amenusurika kuvuliwa uongozi na kupewa onyo  na  na kikao cha mashauriano  cha chama hicho cha Mkoa wa Katavi baada ya kubainika kuwa  amekuwa amekuwa na makundi yanayosababisha mgawanyiko ndani ya chama  na amekuwa akitowa lugha chafu kwa viongozi wenzake .
Mkutano ulioongozwa na Makamu Mwenyekiti Taifa upande  wa Zanzibar Said Mohamed ulifanyika juzi katika ukumbi wa mikutano wa Inyonga Wilyani Mlele .
Mbali ya kikao hicho cha mashauriano cha Mkoa wa Katavi  kumpa onyo Mwenyekiti huyo wa Mkoa  pia kiliwarudisha madarakani viongozi wa chama hicho wa Wilaya ya Mpanda ambao walikuwa wamevuliwa uongozi na wanachama wa chama hicho  kwa kile walichodaiwa kukisaliti chama chao na kupelekea kupoteza jimbo la Mpanda mjini lililokuwa likiongozwa na Said Arfi kwa vipindi viwili  vilivyopita.
Viongozi  waliorudishwa  madarakani ni  Mwenyekiti  Mwenyekiti wa Chama hicho wa Wilaya ya Mpanda Abrahamu Mapunda  ,Katibu wake Idd Faraji  na viongozi wa chadema wa jimbo la Mpanda Mjini.
Wajumbe wa mkutano huo waliamua kuwarudisha madarakani baada ya kubainika kuwa  utaratibu wa kuwaondoa viongozi hao haukufuata taratibu za chama hicho ingawa  kulionekana kuwepo kwa mgogoro ndani ya chama hicho baina ya viongozi na wanachama.
Viongozi wa Wilaya ya Mpanda   ya Mpanda na wa jimbo la Mpanda mjini walisimashwa uongozi  na wanachama wao katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Katavi Resort mjini Mpanda hapo mwezi Novemba mwaka jana  kikao ambacho kiliongozwa na viongozi wao wa kanda ya magharibi na kulikuwa na vurugu kubwa na ulinzi mkali wa askari polisi .
Kwa upande wa mwenyekiti wa Mkoa Laulent Mangweshi  alikuwa na wakati mgumu kutoka kwa wajumbe wa kikao hicho ambao wengi wao walikuwa wakitaka avuliweuongozi kutokana na tuhuma zilizotolewa dhidi yake .
Miomgoni mwa tuhuma hizo ni  kuwa amekuwa  akikigawa chama kwa kuwa na makundi  na amekuwa akiwatolea lugha chafu viongozi wenzake  na amekuwa akikiuka katiba ya chama hicho.
Kikao hicho kiliamua kumpa onyo na kumtaka asirudie tena makosa hayo  na endapo atarudia tena  atavuliwa uongozi bila kusubiri kikao chochote cha kumjadili.
Makamu mwenyeti wa Taifa upande wa Zanzibar Said Mohamed aliwataka wanachama na viongozi wa chama hicho  kurudisha mshikamano ndani ya chama hicho .
Alisema miongoni mwa mikoa ambayo ilikuwa  inafanya vizuri  kwenye maswala ya uchaguzi Mkoa wa Katavi ulikuwa ni mkoa  wa juu lakini sasa hivi miongoni mwa mikoa ambayo imefanya vibaya kwenye matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita mkoa huo ni mmoja wapo .
Mkoa wa  Katavi unajumla ya majimbo ya uchaguzi matano na chama hicho hakikufanikiwa kupata mbunge hata mmoja na  kina madiwani wane katika Mkoa mzima wa Katavi  walipata katika majimbo yam panda vijijiji na Nsimbo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa