Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Manispaa ya
Mpanda Mkoani Katavi
Desemba saba inatarajia kuzindua mpango mkakati wa usafi na utunzaji wa mazingira na upandaji wa miti
Mkurugenzi wa
Manispaa ya Mpanda Selemani Lukanga
aliwaambia waandishi wa Habari juzi ofisini kwake
kuwa uzinduzi huo wa aina yake utafanyika
katika uwanja wa Azimio mjini hapa
na mgeni Rasmi
atakuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi
Dr Ibrahimu Msengi
Alisema
Manispaa hiyo imeweka mpango mkakati wa utunzaji wa mazingira na upandaji wa miti katika
maeneo yote ya Manispaa hiyo ya
Mpanda
Alifafanua
kuwa Manispaa inayo mikakati ya
usafi wa mazingira na
wamekuwa wakiitekeleza na wamekuwa wakipata ushindi wa
Kitaifa wa utunzaji wa mazingira
hivyo wanaenda sambamba na
gizo la Rais John Magufuli
alilo litowa hivi karibuni la
utunzaji wa mazingira
Lukanga
alieleza watatumia uzinduzi
huo kuweza kujipima toka
Halmashauri hiyo ilianzishwa mwaka 2007 ikiwa Halmashauri ya Mji na sasa Manispaa wamefanikiwa kwa kiasi gani katika usafi na utunzaji wa mazingira na pia
wamepanga kujipanga kama Manispaa
kwani hapo awali walikuwa ni
Halmashauri ya Mji na sasa Nimaspaa kuanzia Julai mwaka huu
Alisema
lengo pia la uzinduzi huo ni
kuwafanya wadau mbalimbali waweze
kushiriki kwa vitendo katika shughuli za usafi na utunzaji wa mazingira na
kuwafanya wananchi wapende usafi
Lukanga alieleza siku
hiyo ya uzinduzi wananchi na
Taasisi mbalimbali za
Manispa ya Mpandawatashiriki
kwenye zoezi la kufanya usafi
wakiwa wameongozwa na Mkuu wa
Mkoa wa Katavi Dr Ibrahimu Msengi
Alisema
Mkuu wa Mkoa kwenye uzinduzi
huo atakabidhi pikipiki mbili kwa
Maafisa wa Afya wa Manispaa ya
Mpanda zilizo tolewa zawadi kwa Manispaa hiyo baada ya kuwa
washindi wa utunzaji wa mazingira Kitaifa na pia atakabidhi cheti cha ushindi kwa
kijiji cha Kamakuka kilichopo katika Manispaa ya Mpanda kwa kuwa washindi wa kwanza wa ujenzi
wa vyoo vya kisasa hapa Nchini
0 comments:
Post a Comment