Home » » WANANCHI WASIMAMISHA MSAFARA WA MAGUFULI ILI WAMWONE WAJIPANGA BARABARANI

WANANCHI WASIMAMISHA MSAFARA WA MAGUFULI ILI WAMWONE WAJIPANGA BARABARANI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter Mguluchuma
Katavi
Msafara wa mgombea wa  Urais(CCM) Dk  John  Magufuli  ulilazimika kusimama katika  Vijiji  vitatu  tofauti  hapo  jana wakati ukiwa unatokea Mjini Mpanda kuelekea  Mishamo  wilayani  hapa  baada ya wananchi wa vijiji hivyo waliokuwa wamejipanga kwa wingi barabarani na kuuzuia msafara huu ili waweze kumwona Dk  Magufuli
  Msafara huu wa mgombea Urais ulianza  kusimamishwa  katika  Kijiji cha  Majalila  hali  ambayo ililazimu  msafara huu usimame na  kumfanya Dk  Magufuli aamue  kusimama katika  gari lake  na kuwasalimia wananchi hao na kuwahaidi endapo atachaguliwa  atahakikisha anamaliza  kero za  Wananchi hao kwani zinatambulika
 Hali  kama  hiyo ilitokea tena kwenye  vijiji vilivyokuwa mbele vya  Nkondwe na  Luhafe  ambako alikuta wananchi wakiwa wamejipanga kwa wingi kando ya barabara huku wakiwa na shauku ya kumwona  hari ambayo ilipelekea  msafara huu usimame na  Dk  Magufuli kulazimika kusimama na kuwahutubia mamia ya wananchi hao walikuwa wamesimama kando ya  barabara
Mgombea  huyo wa Urais(CCM) alipokuwa akiwahutubia maelfu ya Wananchi  waliokuwa  Raia wa Nchi ya Burundi ambao wamepewa Urai wa Tanzania  katika Kijiji cha Mishamo  aliwahakikishia kuwa  Serikali yake  ijayo ya awamu ya  tano itahakikisha inawaboreshea  miundo mbinu mbalimbali
 Alisema  Serikali yake  itajenga barabara kwa kiwango cha  rami  barabara yenye urefu wa kilometa 199 inayotoka Mpanda  hadi uvinza Mkoani  Kigoma
Pia itajenga  zahanati kila kijiji na kila kata  atahakikisha wanajenga kituo cha afya na kila Wilaya Hospitali   na kila Mkoa  Hospitali ya Rufaa
Vilevile Serikali yake itatowa elimu bure kuanzia  shule ya Msingi hadi sekondari  na itaboresha  makazi ya  nyumba za kuishi waalimu na itaboresha huduma ya maji na  kufikisha nishati ya umeme kwa yale maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa