Home » » MAUAJI: MWANAUME AMCHOMA VISU MPENZI WAKE MPAKA KUMUUA KISHA NA YEYE KUJICHOMA VISU TUMBONI HADI KUTOKA UTUMBO NJE.

MAUAJI: MWANAUME AMCHOMA VISU MPENZI WAKE MPAKA KUMUUA KISHA NA YEYE KUJICHOMA VISU TUMBONI HADI KUTOKA UTUMBO NJE.



Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi yetu Blog
 Mwanamke mmoja aliyefahamika  kwa jina la Cecilia  Clement (20) Mkazi wa Mtaa wa Majengo  Wilaya ya Mpanda  ameuwawa  kwa kuchomwa  visu  katika maeneo ya  tumboni  kifuani  na shingoni  na mpenzi  wake  Denson Kanubo (23)Mkazi wa Mtaa huo ambae nae  alijichoma  vifu  vitatu tumboni  na utumbo wake kutoka nje
Kwa mijibu wa Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari  tukio hilo lilitokea hapo june 29 mwaka huu majira ya saa tatu asubuhi
Marehemu   na Denson  walikuwa wakiishi  kwenye nyumba moja  ya dada yake  aitwaye  Priisca  Alex  ambapo  Denson alikuwa ni mpangaji katika nyumba hiyo  na walikuwa na mahusiano ya kimapenzi
Kamanda Kidavashari alisema  hivi  karibuni  watu hao waliingia  katika mtaruku  baada ya dada wa marehemu kubaini mahusiano yao ya kimapenzi  hivyo alitaka marehemu  aachane  na Denson
Alisema siku moja  kabla ya tukio la mauwaji hayo  kulikuwa   na malumbano ya  wapenzi hao wawili  kupitia ujumbe  mfupi  wa simu  ya mkononi  walitumiana  mara 26
 Katika ujumbe huo  marehemu  alikuwa  akimtukana  matusi ya nguoni  na pia marehemu  alikuwa akimhusisha Danson  na biashara ya meno ya Tembo  katika meseji zake  na kwamba siku zake za kukamatwa  zimekaribia
Kidavashari alieleza  Ndenson  alikasirishwa na kitendo hicho cha kutumiwa meseji aliamua  kwenda kumwamsha  dada yake na mareu  na kumwelezea jinsi alivyotukanwa
Alisema siku ya tehehe 29 baada  wapenzi hao kuwa wameamka  waliendelea kutishiana kuchomana visu  na ujumbe wa mwishi wa marehemu  aliomwandikia Danson  ulikuwa ni huu  nanukuu  POA TUU  UNICHOME  KISU  NICHOME UNAOUWEZO  WA KUNICHOMA  KISU  MIMI WEWE....
Wakati dada wa marehemu  akiwaanaendelea na shughuli zake za usafi wa nyumba  alisikia  maarehemu akipiga  kelele  za kuomba msaada huku akilia nakufa  nakufa niachie
Dada  wa marehemu alijaribu kuingia  ndani   ya chumba  na ndipo aliposhudia mdogo wake akiwa anachomwa visu  na yeye mwenyewe  alitishiwa kuchomwa visu endapo athubutu kuingia ndani ya chumba hicho
Ndipo alitoka nje  na kwenda  kuomba msaada  kwa majirani  ambao walifika  na kukuta  tayari Cecilia   ameisha kufa  kwa kumchoma visu  nae akiwa amejichoma vifu  tumboni haadi utumbo kutoka nje
Jeshi la polisi lilifika kwenye eneo hilo na kufanya jitihada za kuokoa maisha ya majeruhi  huyo  na kufanikiwa kumkimbiza kwa ajiri ya matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda  ambako amelazwa na hari yake   inaendelea vizuri   kidogo
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa