Home » » DC AWATAKA VIJANA KUJIUNGA NA VETA

DC AWATAKA VIJANA KUJIUNGA NA VETA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter Mguluchuma
Mpanda Ka tavi
Mkuu wa  Wilaya ya Mpanda Paza  Mwamlima  amewataka  vijana  kujiunga  na mafunzo  ya  VETA kuanzia  waliomaliza elimu ya Msingi  ili  wakape  wawaze  kupata  elimu ya kujiajiri
Mwamlima alitowa wito huo hapo juz kwenye Kijiji cha Kasekese  Wilayani  hapa       wakati akifungua kambi ya vijana walijitolea     kufyatua matofali kusomba  mawe na mchanga  kwa ajiri ya ujenzi wa  vyumba vya madarasa kumi ya shule ya Msingi ya Kasekese  na bweni la sekondari ya Mpanda Ndogo
Alisema     vijana wanawajibu wakutambua kuwa  Taifa  la Tanzania  linawategemea  vijana kwa ajiri ya ujenzi wa nchi na sio wao kulitegemea  Taifa
Aliwafafanulia kuwa  mataifa yote Duniani  yanajengwa  na yalijengwa  na vijana  hivyo  wanawajibu wa kuutumia vizuri ujana wao kwa sughuli za ujenzi wa Taifa
Alisema  vijana wa Wilaya ya Mpanda wanayonafasi kubwa  ya kuanzisha  shughuli  za kiuchumi  kutokana na furusa  zilizopo Wilayani hapa
Alifafanua vijana wengi katika Wilaya ya Mpanda hawana ardhi  hivyo  vijiji  vyote  vikae  na kuwapatia  ardhi vijana zoezi hilo  lifanyike kwa ushirikiano baina ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda na vijiji husika
Alieleza  wako baadhi  ya vijana  wamekuwa wakimshangaa  pale anapokuwa  akiongelea vijana  wapewe ardhi wanapaswa watambue kuwa  rasilimali  kubwa ya bara la Afrika ambayo ni yauhakika ni  ardhi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa