Home » » ASKOFU NYAISONGWA ASIMIKWA KUWA ASKOFU WA JIMBO LA MPANDA

ASKOFU NYAISONGWA ASIMIKWA KUWA ASKOFU WA JIMBO LA MPANDA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na Walter Mguluchuma
Mpanda  Katavi
Askofu Gervas  Nyaisonga  amesimikwa   kuwa Askofu wa Kanisa  Katoliki  Jimbo la Mpanda  ambalolilikuwa wazi  kufutia kifo cha aliyekuwa Askofu  wa jimbo hilo  Askofu Wiliamu  Kikoti  aliyefariki  Dunia  tarehe  28 Agosti  2012
Ibada ya kusimikwa Askofu  Gervas Nyaisonga  ilifanyika juzi   kwenye  viwanja  vya shule ya chekechea  inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda ambayo ilihudhuriwa  na maaskofu  wapatao ishirini  wa majimbo mbalimbali na viongozi wa Serikali akiwemo  Mke wa Waziri  Mkuu  Tunu  Pinda
Askofu  Gervas Nyaisonga   aliteuliwa na Baba mtakatifu  Francisko  1 kuwa Askofu wa jimbo la Mpanda  hapo mwezi februai  mwaka huu  kabla ya  uteuzi huo  i Askofu Gervas Nyaisnga  alikuwa ni  Askofu   wa Jimbo la Dodoma  ambalo   ambalo  ameliongoza jimbo hilo kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2011
Katika  salamu zaBaraza  la Maskofu  zilizotolewa na  Rais wa  Baraza  la Maaskofu Tanzania  Askofu Taransiunce  Ngalalekumtwa  alieleza kuwa   Baraza la maaskofu  linaimani na Askofu Nyaisonga kuwa  anao uwezo mkubwa wa kuliongoza jimbo la mpanda hivyo hawana mashaka  na uteuzi huo wa kuhamishiwa kwake kuwa Askofu wa jimbo hilo
Alisema   Waumini wa kanisa hilo  wa jimbo la Mpanda  na wanachi   wanawajibu wa kumpa  ushirikiano Askofu Nyaisonga ili  aewze kufanya kazi zake vizuri  
Kwa upande wake mke wa  waziri mkuu Mama Tunu Pinda  alieleza kuwa anamfahamu  vizuri Askofu Nyaisonga kuwa ni mpenda  maendeleo  sana  na mpenda watu  hivyo wanampanda  watarajie  yale ambayo yalikuwa yameanzishwa  na marehemu Askofu Kikoti yataendezwa nae  hivyo kiatu alichokiacha  Askofu Kikoti  kimepata mvaaji ambae ni Askofu  Nyaisonga Alisema  Tunu Pinda
Aidha  Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Rajabu  Rutengwe  alieleza kuwa  Mkoa  wa Katavi unarasilimali  nyingi  lakini unakabiliwa  na changamoto mbalimbali  ambazo zinahitaji ushirikiano wa Serikali na kanisa ili kuweza kuzipunguza na kuzimaliza
Dr Rutengwe alizieleza  baadhi ya changamoto hizo ni miundombinu mibovu ya barabara  eimu na   Afya  ambapo mkoa wa Katavi  mpaka sasa hauna hospitali yake ya Mkoa  wanategemea Hospitali ya Wilaya ya Mpanda  tuu

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa