Home » » Serikali yaombwa kusimamisha utoaji wa vitalu vya uwindaji wanyama ili kupnguza ujangili.‏

Serikali yaombwa kusimamisha utoaji wa vitalu vya uwindaji wanyama ili kupnguza ujangili.‏

N a Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi yetu blog
Taasisi ya  umoja wa Wabunge  inayoshughulikia  uhifadhi wa  wanyama pori na mistu  wameiomba  Serikali  kusimamisha  utoaji wa  vibali vya vitalu kwa ajiri ya uwindaji wa wanyama pori na  vibari  vya uchimbaji wa madini kwenye maeneo ya yanayopakana karibu na Hifadhi za Taifa  kutokana  na baadhi  ya makampuni hayo  kutumia maeneo hayo kwa ujangili wa Tembo na Falu
 Hayo yamesemwa hapo juzi  kwa nyakati tofauti na  Mwenyekiti wa  Taasisi hiyo Riziki  Lulida wakati akizungumza na Mkuu wa  Mkoa wa Katavi Dokta  Rajabu  Rutengwe  ofisini kwake na wakati  alipokuwa akizunguza na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya  wanyama pori ya Katavi  pamoja na watumishi wa pori  la Akiba la  Rukwa Rukwaki katika chuo cha wanyama pori cha Mlele
Lulida alielezakuwa   yapo makampuni  ya kigeni ambayo  yamepewa vibali  vya vitalu vya uwindaji  na uchimbaji wa madini  wamekuwa wakitumia vibari hivyo vibaya  na matokeo yake  wamekuwa wakijihisisha  na uwindaji haramu wa Faru na Tembo  hivyo ni vizuri Sekari ikasitisha  walau  utoaji wa vibali hivyo kwa kipindi cha miaka kumi
Alisema  Wanyama  wetu wako hatalini kupotea  na utalii utakuwa umekufa kabisa  hesabu ya  mwaka 2000 inaonyesha Tanzania ilikuwa na jumla ya Tembo  milioni mbili lakini waliopo sasa  ni elfu kumi na tatu tuu
Kwaupande wake makamu mwenyekiti wa Taasisi hiyo ya Bunge Mwandisi Athuman Mfutakamba  alieleza endapo hatua mahususi za haraka hazita chukuliwa  utalii wan chi  utakufa  na watu watakuwa wanaenda kuona wanyama kwenye nchi za wenzetu  na pato letu la uchumi litapungua kwani utalii unachangia asilimia 21  . 7 ya pato la taifa
Alifafanua kuwa lengo la  taasisi  hiyo ni pia ni kuwapa wananchi  wanaojihusisha na ujangili  uwelela  wa umuhumu  wa uwifadhi  wa wanyama pori kwa faida  za sasa na kwa siku zijazo
Aidha Katibu  mkuu wa taasisi hiyo  Silvester Mabumba  alieleza kuwa ni vizuri Serikali  ikaongeza umakini zaidi  kwa kutowaamini  kupita  kiasi Raia wa kigeni  kwani baadhi yao wamekuwa wakijihusisha  na ujangili wa wanyama wetu  na kuharibu mistu kwa kujihusisha na biashara za magogo ya miti
Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Dr Rutengwe  alisema  Hifadhi zetu za wanyama  hazina mipaka inayo onekana  hivyo  imekuwa  ikichangia  sana  uharibifu wa mazingira na kuongezeka kwa ujangili
Alisema ili  kukabiliana na wimbi la  ujangili  lililipo kwa sasa  ni muhimu  Hifahi  zote zikawa    na vifaa vya kisasa  na mawasiliano ya uhakika
Nao  watumishi wa Hifadhi ya Katavi na wapori la akiba la Rukwa RUkwati walieleza kuwa  katika  majangili wanaokamatwa katika maeneo  yao   asilimia sabini ni raia wa kigeni wa Nchi ya Burundi
Pia walieleza kuwa  wamekuwa  wamekuwa wakikabiliwa na tatizo la upungufu wa watumishi  na uchache wa magari  kutokana na mbuga hiyo ya Katavi kuwa na kilometa 4771 za mraba hivyo wanahitajika watumishi wakutosha na magari ilikukabiliana na  ujangili

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa