Home » » Akina baba watakiwa kutoa Taarifa polisi wanapopigwa nawake zao wasione aibu.

Akina baba watakiwa kutoa Taarifa polisi wanapopigwa nawake zao wasione aibu.

N a Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi yetu blog
Mkuu wa Kitengo kitengo cha Dawati la unyanya wa jinsia wa  jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Mkaguzi wa  wa Jeshi la polisi  Viliginia  Sodoka  amewataka  akina baba wa Mkoani hapa  kuacha tabia ya kutopeleka  mashitaka yao polisi  pindi wanapo  pigwa na wake zao
Sodoka alitowa kauli hiyo hapo juzi  kwenye wodi ya wagonjwa  ya wanaume  wakati akizungumza na wagonjwa waliolazwa kwenye wodi hiyo alipo watembelea  na kuwafariji ikiwa ni katika sehemu ya  siku kumi na sita  ya kuhamasisha kupinga unyanyansaji wa jinsia
Katika ziara hiyo ya kutembelea hospitali ya Wilaya ya Mpanda  kitengo hicho   kilitowa msaada  wa  sabuni , biscuti na  vinywaji baridi  kwa wagonjwa waliolazwa katika wodi mbalimbali  vikiwa na thamani ya shilingi laki tatu na nusu
Mkuu huyo wa kiteno cha  dawati la jinsia na unyanyansaji wa jinsia alieleza kuwa  wapo wanaume wengi wamekuwa  wakifanyiwa vitendo  vya unyanyansaji na wake zao  baadhi yao wamekuwa wakipigwa na wake zao lakini wamekuwa wakiona aibu kwenda polisi kufungua mashitaka
Sodoka aliwaeleza acheni kuona  kuona aibu mnapo nyanyaswa  na wake zenu  dawati la  unyanyansaji wa jeshi la polisi  lipo wazi  muda wote kusikiliza na kutatua  matatizo hayo ya unyanyasanji wa kijinsia
Kwa upande wake  Mganga mkuu wa Hospital ya Wilaya ya Mpanda Dokta  Nasibu Mkongwa  alishukuru msaada huo uliotolewa na kitengo hicho cha polisi kwani kitawafariji wagonjwa kwani baadhi yao ndugu zao wako mbali 
Pia  ametowa wito kwa taasisi  nyingine mkoani hapa kuiga mfano  wa kitengo cha polisi  cha dawati la unyanyansaji wa kijinsia  kwa msaada huo kwa wagonjwa na wao waige mfano huo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa