Home » » HALMASHAURI ZATAKIWA KUWASHIRIKISHA WANANCHI WAKE KWENYE MIPANGO YA MAENDELEO‏

HALMASHAURI ZATAKIWA KUWASHIRIKISHA WANANCHI WAKE KWENYE MIPANGO YA MAENDELEO‏

N a Walter Mguluchuma
Mpanda  Katavi
Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Dokta Rajabu Rutengwe  ametowa wito kwa Wakuu wa Wilaya na  na Wakurugenzi wa Halmashauri  wa Mkoa wa Katavi kuhakikisha  wanawashirikisha wananchi  katika kupanga  na kutekeleza  mipango ya maendeleo  katika  Wilaya zao
Wito huo aliutowa hapo juzi wakati akiwahutubia Wananchi wa Tarafa ya usevya  kwenye mkutano wa hadhara wa  kwenye kilele  cha maadhimisho ya sherehe  za miaka  52 ya Uhuru  zilizofanyika kimkoa katika Tarafa ya Usevya Wilaya ya Mlele
Dokta Rutengwe  alisema  Halmashauri za Mkoa wa  katavi  zinatakiwa  zinawashirikishe wananchi wake  katika kupanga mipango ya maendeleo  ambayo  italenga  katika kumwondolea  mwananchi umasikini  na ziwe tayari kupeleka madaraka kwa mwananchi
Alieleza  Halmashauri  ziwe  ni vyombo harisi  vya  wananchi na viwajibike kwa wananchi  katika utendaji wake wa shughuli zote ambazo zinahusu maendeleo katika  Halmashauri husika
Aidha alieleza  Vijana kama  nguzo  ya rasilimali  ya Taifa  letu  ni vizuri wakawekewa  mikakati  thabiti  ya kuwainua  kielimu  na kimaendeleo kwa ujumla
Endapo  Haimashauri  zitawasahau  vijana  katika  mipango  yao  zitambue  kuwa  zitalitumbukiza  Taifa  kwenye hatari ya   matukio mbalimbali  kama vile wizi ,utapeli  ujambazi  na kuenea  kwa magonjwa  kama vile Ukimwi
Pia alieleza kuwa katika kipindi ca miaka 52 ya Uhuru  Mkoa wa Katavi  umepata mafanikio katika  sekta  mbalimbali za maendeleo  ambazo
Alisema  wakati wa Uhuru mkoa wa Katavi ulikuwa na  shule za msingi sita  na sekondari  kulikuwa  hakuna shule ya sekondari hata moja ambapo baada ya miaka 52 ya Uhuru Mkoa wa Katavi unashule  za msingi  194 na shule za Sekondari 37  na chuo kimoja cha VETA  na chuo cha maendeleo  ya jamii kimoja  na Serikali ipo mbioni  kuanza ujenzi wa chuo  kikuu cha kilimo   cha Katavi
Upande wa Afya Mkoa  una hospitali moja Vituo vya afya kumi na tatu  na zahanati zilizopo ni  61 hali hii ni nzuri ukilinganisha na wakati wa uhuru  ilivyokuwa  ambapo vituo vya Afya  na zahanati havikuwepo kwenye maeneo ya vijiji alisema DR Rutengwe
Alisema huduma ya maji imeboreshwa ambapo wakati wa Uhuru asilimia moja ya wananchi katika mkoa wa Katavi ndio walikuwa wakipata maji safi na salama  ambapo  kwa sasa asilimia arobaini na nane  ya watu 271.010 ya wakazi wa Mkoa wa Katavi  wananufaika na maji safi na salama   lengo la Mkoa na Taifa  kwa ujumla  ni kufikia asilimia sitini na saba
Maadhimishi ya sherehe hizo  yalitanguliwa na upandaji  wa shamba darasa namba moja la mkoa wa Katavi la Waziri Mkuu Mizengo Pinda lililoko  katika kijiji cha Kibaoni ambapo wanachi walijifundishwa namna ya kilimo bora cha kisasa  na kupanda mbegu bora  za mahindi kwa mstali
Pia zoezi hilo la upandaji wa mahindi liliwashirikisha viongozi mbalimbali wa Mkoa wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa  na viongozi wa wilaya za Mpanda na Mlele

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa