Home » » WAWILI WAKAMATWA NA NYARA ZA SERIKALI NGOZI YA CHUI YA THAMANI YA SH. MILIONI 10‏

WAWILI WAKAMATWA NA NYARA ZA SERIKALI NGOZI YA CHUI YA THAMANI YA SH. MILIONI 10‏

Na Walter Mguluchuma-Katavi yetu blog
Mpanda-Katavi
Jeshi la polisi mkoa wa Katavai kwa kushirikiana na askari wa hifadhi ya Taifa ya Katavi wamewakata watu wawili wakiwa na nyara za serikali ngozi ya chui mbili zenye thamanai ya zaidi ya milioni 10.
Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Katavi kamishina msaidizi Emmanuel Nlay aliwataja waliokamatwa ni Komanya Luponya (28) mkazi wa kijiji cha Mbede wilaya ya Mlelel na Heleni Jilala (20) mkazi wa Muzye Sumbawanga mkoani Rukwa
Alisema watuhumiwa hao walikamatwa Mei 22 mwaka huu majira ya saa moja asubuhi katika eneo la kijiji cha Mwamadulu tarafa ya Mpimbwe wilaya ya Mlele mkoa wa katavi.
Watuhumiwa hao walikamatwa kufuatia taaraifa zilizokuwa zimelifikia jeshi la polisi kuwa watu hao wanajihusisha na uwindaji haramu katika hifadhi ya taifa ya katavi.
Nlay alieleza polisi kwa kushirikiana na askari wa ifadhi ya katavi walifanikiwa  kuwakuta watuhumiwa wakiwa kwenye kambi waliyofikia ambayo ilikuwa ni kwa ajili ya malisho ya ng’ombe.
Baada ya kupkuliwa watuhumiwa walikutwa na nyara za serikali ngozi mbili za chui zenye thamani ya shilingi Tsh. 10,500,000/=
Kaimu kamanda Nlay alieleza watuhumiwa watafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi kuwa umekamilika ili waweze kujibu mashitaka ya kukamatwa  na nyara za serikali.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa