Home » » POLISI WA KAMATA BANGI DEBE MOJA NA KETE 163 ZA BANGI‏

POLISI WA KAMATA BANGI DEBE MOJA NA KETE 163 ZA BANGI‏

Na Walter Mguluchuma
Mpanda
Jeshi la polisi mkoa wa  katavi lina washikilia watu watatu kwa tuhuma za kuwakamata na  Bangi katika matukio mawili tofauti likiwemo la mtu mmoja kukamatwa na debe moja la Bangi lenye uzito wa kilo tano.
Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa katavi Emanuel Nlay alisema katika tukio la kwanza polisi waliwakamata  watu wawili David Sumun (54) na Joseph Peter (30) wote wakazi wa kijiji cha Dilifu wilaya ya mlele wakiwa na Bangi kete 163 zenye uzito wa Gram 815
Watuhumiwa hao walikamatwa hapo Mei 16 Mwaka huu majila ya saa 8 mchana  katika kijiji cha Dilifu kufutia msako uilio fanywa na polisi kwa kushilikiana na sungusungu wa kijiji hicho.
Katika tukio la pili polisi wamemkamata January Katambala (33) mkazi wa kijiji cha Mtisi wilaya ya mlele alikamatwa akiwa na Dawa za kilevya aina ya Bangi debe  moja yenye uzito wa kilo tano
kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Katavi Emanuel Nlay alisema mtuhumiwa alikamatwa  hapo mei 25 Mwaka huu majira ya saa 12 Jioni akiwa nyumbani kwake.
Alisema mtuhumiwa  alikamatwa kufutiwa taarifa ambazo zilikuwa zimelifikia Jeshi la hilo kuwa mtuhumiwa amekuwa  akijiusisha na Biashala haramu ya kununua na kuuza Bangi.
Baada ya tarifa hizo polisi walianza uchunguzi na ndipo ilipo timia siku hiyo  ya tukio walipo weza kufanikiwa kukamata mtuhumiwa akiwa na Bangi hiyo  aliyokuwa amehifadhi ndani ya nyumba yake.
Nlay amesema watuhumiwa hao wote watatu wanatarajiawa kufikishwa mahakamani wakati wowote mara baada ya upelelezi kufanyika. 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa