Home » » AJIUA KWA KUNYWA VIDONGE BAADA YA KUKUTWA NA VIRUSI VYA UKIMWI‏

AJIUA KWA KUNYWA VIDONGE BAADA YA KUKUTWA NA VIRUSI VYA UKIMWI‏

Na Walter Mguluchuma-Katavi yetu Blog
Mpanda
Mkazi wa mtaa wa Kotazi wilayani Mpanda mkoa wa Katavi BARAKA Mtaki (32) amejiua kwa kunywa vidonge baada ya kupimwa afya yake na kukutwa na maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.
Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Katavi kamishina msaidizi Emmanuel Nlay alisema tukio hili limetokea Mei 24 mwaka huu majira ya saa 10 jioni nyumbani kwa marehemu.
Alisema siku hiyo ya tukio marehemu Baraka alikunywa vidonge vya maralia aina ya mseto vidonge 12 na frajili sita kwa wakati mmoja akiwa chumbani kwake.
Marehemu alikunya vidonge hivyo baada ya mkewe aitwae Tatu Philipo (32) kuondoka nyumbani na kuelekea mashineni kusaga unga.
Kaimu kamanda Nlay alieleza baada ya mkewe tatu kurudi nyumbani na alipoingia ndani alimkuta marehemu akiwa amelala huku povu likimtoka mdomoni na alipojaribu kumsemesha hakuweza kumuitikia.
Tatu baada ya kuona hali hiyo ilimlazimu aombe msaada kwa majirani ambao walifika katika eneo hilo
Nlay alieleza baada ya majirani kufika hapo waliamua kumchukua marehemu na kumkimbiza katika hospitali ya wilaya ya Mpanda wakati wakimwinua kitandani waliweza kuona pembeni alipokuwa amelala pakiwa na paketi mbili za adawa ya maralia aina ya mseto zikiwa zimebaki paketi tupu na vidonge sita vya Frajili vilivyokuwa vimeachwa na mkewe navyo vikiwa paketi tupu.
Marehemu alipofikishwa katika hospitali ya wilaya ya mpanda alifariki baada ya muda si mrefu wakati akiwa amekwisha anza matibabu .
Kaimu kamanda alieleza hivi karibuni marehemu  alipoona anasumbuliwa na maradhi ya mara kwa amara aliamua kwenda kupimwa afya yake na ndipo alipokutwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi.
Kutokana na hali hiyo marehemu aliweza  kuwaambia rafiki zake pamoja na mkewe kuwa ktokana na kugunduliwa yeye na virusi vya ukimwi ni bora siku moja ajiue kwa kunya vidonge kuliko kuendelea na mateso ya maradhi.


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa