Na Walter Mguluchuma-Blogs za Mikoa
Mpanda
Wananchi wa kijiji cha Kapanda kata ya mashimboni wilayani Mlele Mkoa wa Katavi wanakabiliwa na tatizo la ukosefu wa huma ya afya kutokana na kutokuwepo kwa Zahanati kijijini hapo kutokana na Halmashauri ya wilaya ya Mpanda kushindwa kukamilisha jengo la zahanati kwa kipindi zaidi ya miaka kumi na moja.
Kutokana na tatizo hilo wajumbe wa kamati ya ARAT ya wajumbe wa kukagua miradi ya mikoa ya Rukwa na Katavi ilitembelea jengo la zahanati hiyo hapo novemba mwaka jana na kuigiza Halmashauri ya wilaya ya Mpanda inakamilisha ujenzi wa jengo hilo mapema iwezekanavyo.
Makamu mwenyekiti wa ARAT wa mikoa Ya Katavi na Rukwa Enock Gwambasa jana akiwa na wajumbe wawili wa walifika kijijini hapo ili kukagua ujenzi wa zahanati hiyo iliyo jengwa kwa nguvu ya wananchi kwa kushirikiana na hifadhi ya wanyama pori ya Rukwa rukwati na Halmshauri ya wilaya ya Mpanda iliyo pewa jukumu la kumalizia hatua ya mwisho ya jengo la zahanati lililoanza kujengwa toka mwaka 2002 ziara hiyo waliifanya hapo jana.
Gwambasa alisema amesikitishwa na kitendo cha Halmashauri ya wilaya hiyo kushindwa kukamilisha ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho lisha ya kuwa maagizo yalisha tolewa.
Alieleza hari inaweza ikasababisha wahisani wanao towa misada ya ujenzi wa miradi wakate tamaa kutokana na kuchelewa kwa miradi wanayo saidia.
kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Justine Tibelanda aliwaeleza wajumbe wa kamati hiyo ya ARAT kuwa Halmashauri itajitahidi kukamilisha ujenzi wa zahanati hiyo.
Nae afisa mtendaji wa kata hiyo John Wambulu alieleza kuwa kijiji hicho kina jumla ya kaya 420 na wananchi wamekuwa wakitembea umbali wa zaidi ya kilometa 20 kwenda kupata huduma za afya katika zahanati ya kata ya Magamba.
Alisema endapo jengo la zahanati hilo lingekuwa limekamilika wananchi wa kijiji hicho ambacho ni maarufu kwa uchimbaji wa dhahabu wangeondokana na usumbufu wa kutembea umbali wa muda mrefu kutafuta huduma ya matibabu .
kwa upande wake kaimu afisa mtendaji wa kijiji Jeturuda Kilimanjaro alieleza kuwa jengo hilo limeanza kuchakaa kutokana na wananchi kulifanyi usafi kwa muda mrefu na sasahizi wamekatishwa tamaa kuona jengo hilo halikamiliki na wao kuanza kupatiwa huduma katika zahati ya kijiji chao.
0 comments:
Post a Comment