Jiunge na Huduma ya Tone Mobile News Bure kabisa kupitia Whatsapp yako na uwe wa kwanza kupata kile kinachotokea ni Rahisi sana Ingia katika uwanja wa kuandika ujumbe mfupi wa maneno katika Whatsapp yako kisha andika TONE MOBILE NEWS tuma kwenye namba 0756364660 utapokea ujumbe kuwa umeunganishwa.
Na
walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Shirika la
nyumba la Taifa
(NHC) limekabidhi msaada wa
mashine kumi na mbili
za kufyatulia matofali kwa vijana wa
Halmashauri za Mkoa wa
Katavi zenye jumla ya
zaidi ya shilingi
milioni tano pamoja na fedha
tasilimu shilingi milioni mbili
Msaada huo
ulikabidhiwa hapo jana kwenye
hafla iliyofanyika kwenye
ukumbi wa Idara
ya maji ulioko
mjini hapa ambapo
mgeni Rasmi wa
hafla hiyo alikuwa
Mkuu wa Mkoa wa
Katavi Dr Rajabu
Rutengwe
Meneja wa
Shirila wa shirika
la nyumba wa Mkoa
wa Katavi Nehemia
Msingwa alieleza kwenye hafla
hiyo shirika hilo
limetowa msaada wa
mashine kumi na mbili
kwa vikundi vinne
vilivyoko katika Halmashauri za Mpanda
mjini , Nsimbo na Halmashauri
ya Wilaya ya
Mpanda zenye jumla ya
thamani ya Tsh 5,600,000
Alifafanua
kila Halmashauri imepatiwa
mashine nne kutoka NHC
isipo kuwa Halmashauri ya mji wa
Mpanda ambayo imepata mashine sita
ambapo mashine mbili zimenunuliwa kwa pesa tasilimu
na Halmashauri hiyo ikiwa
imeanza kutekeleza agizo la waziri mkuu
la kuzitaka kila Halmashauri
kutenga fungu maalumu kwa ajili
ya kununulia mashine hizi
Alisema shirika la NHC kwa
kushirikiana na chuo
cha ufundi stsdi
VETA Mpanda kimewaandalia
mafunzo vijana wa vikundi hivyo
namna ya kuzitumia mashine hizo
na ndio maana NHC imewapatia kila
kikundi kiasi cha
Tsh 500,000 kwa kila
kikundi kama sehemu ya mtaji ambao
wanatakiwa wautumie mara baada ya
kumaliza mafunzo
Msingwa alieleza
Shirika la NHC
limebuni mpango huu
mahsusi kwa ajiri ya
kuwasaidia vijana mashine za kufyatulia matofali
na utakuwa ni endelevu
ilikuwasaidia vijana kujiajiri wenyewe na kupunguza tatizo
la ajira
Mgeni
Rasmi wa hafla hiyo
Dr Rajabu Rutengwe
alisema Serikali ya
Mkoa wa Katavi inatambua
juhudi zinazofanywa na NHC
toka wamefika katika
Mkoa huu kumekuwa na
mabadikliko makubwa ya
kimaendeleo
Alisema ni vizuri
vikundi hivyo vilivyopatiwa msaada huo kuhakikisha vinatumia hurusa
hiyo vizuri na wajitume kwenye
elimu wasijione kama wamechelewa
Rutengwe
pia aliwahimiza wazazi
wawekeze watoto wao kwenye
swala la Elimu
hivyo wazazi wahakikishe wanawasomesha watoto wao ambao hawakwenda Sekondari wawapeleke kwenye shule za ufundi
Mkuu wa Mkoa
aliziagiza Halmashauri zote za Mkoa
wa Katavi zihakikishe
zinatenga maeneo kwenye Halmashauri
zao kwa ajiri ya ujenzi
wa nyumba za
Shirika la Nyumba
la Taifa
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Home »
» SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA LA TOA MSAADA WA MASHINE ZA KUFYATULIA MATOFARI KWA VIJANA WA MKOA WA KATAVI
0 comments:
Post a Comment