Home » » Mitishamba ya kuongeza uchungu yaua wanawake

Mitishamba ya kuongeza uchungu yaua wanawake

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


WILAYA ya Mpanda mkoani Katavi inakabiliwa na changamoto ya wajawazito kufa kutokana na kutumia dawa za miti shamba kuongeza uchungu wakati wa kujifungua.
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mpanda , Dk Naibu Mkongwa alikiri kuwa vifo vya wajawazito hospitalini hapo vinasababishwa na matumizi ya dawa za kienyeji.
Alisema asilimia 90 ya wajawazito wanaokaribia kujifungua wanatumia miti shamba kwa siri kujiongezea uchungu wa uzazi jambo linalohatarisha maisha yao.
Alibainisha hayo hivi karibuni mbele ya wajumbe wa CCM wa Umoja wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) wakiongozwa na Mbunge wa Viti Maalumu wa mkoa wa katavi , Anna Lupembe.
“Changamoto kubwa ni kuongezeka kwa idadi ya vifo vya wajawazito kila mwezi kati ya vifo viwili hadi vinne lakini kwa wastani vitatu. Nakumbuka mwaka 2012 kulikuwa na vifo 40 vya wajawazito. “Nisiwe mwongo vifo hivyo vyote vingeweza kuzuilika, tatizo kubwa lililopo wananchi wengi wanaamini dawa za kienyeji kuliko dawa zetu, asilimia 90 ya wajawazito wanatumia dawa za miti shamba wanaposubiri kujifungua ili wapate uchungu wa haraka,” alisema Dk Mkongwa.
Kuthibitisha hilo, alisema hivi karibuni walimkamata mhudumu wa afya aliyekuwa akisubiri kujifungua hospitalini hapo akitumia dawa za miti shamba za kuongeza uchungu wa uzazi.

Chanzo Gazeti la Habari leo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa