Home » » POLISI KATAVI WAKAMATA SILAHA MBILI ZA KIVITA NA RISASI 62 NA GOBORE MBILI

POLISI KATAVI WAKAMATA SILAHA MBILI ZA KIVITA NA RISASI 62 NA GOBORE MBILI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter Mguluchuma
  KATAVI YETU BLOG
Jeshi la Polisi Mkoani Katavi  limekamata silaha mbili za kivita  aina ya  SMG  zikiwa na jumla ya risasi 62 na magazeni mbili  pamoja na bunduki mbili aina ya gobore kabla  ya kufanyika kwa   tukio la ujambazikatika mnada wa mifugo ya ng-ombe  katika Kata ya Simbesa Wilayani Mpanda .
Kaimu kamanda wa polisii wa Mkoa wa Katavi Rashid Mohamed aliwaambia waandishi wa Habari hapo jana kuwa tukio hilo lilitokea hapo jana majira ya saa tatu  asubuhi huko katika kijiji cha  Smbesa kata ya Simbesa.
 Alisema watu wawili wanaosadikiwa kuwa majambazi  wakiwa na pikipiki moja  aina ya  Huonian rangi nyekundu  yenye namba za usajiri  T.948 BHU wakiwa wamebeba  tenga la kubebea mizigo nyuma ya pikipiki walikutana na askari polisii wa doria.
Kaimu kamanda alieleza  waliposimamishwa na porisi  walikaidi agizo hilo na walianza kukimbia kwa kutumia pikipiki yao hiyo.
 Askari baada ya kuona wamekaidi amri hiyo walianza kuwafukuza na walipokaribia kuwakamata  walitelekeza pikipiki yao  na kukimbia na kutokomea  kusiko julikana kichakani .
Pikipiki hiyo baada ya kukaguliwa ilikutwa  ikiwa na silaha mbili za kivita aina ya SMG  huku  zikiwa na  risasi 62 na magazine zake zikiwa  zimeviringishwa  kwenye suruali ya jens na kufungwa kwenye tenga  nyuma ya pikipiki.
Kaimu Kamanda  Rashid Mohamed alisema watu hao walikuwa wamepanga kwenda kufanya  ujambazi katika  mnada wan g-ombe ambao ulikuwa ukifanyika katika kijiji cha  Simbesa.
Katika tukio jingine lililitokea hapo juzi katika kijiji hicho cha Simbesa  mtu mmoja alijulikana kwa jina la  Ge4ofrey  john 34 Mkazi wa Kijiji cha  Nkungwi  alikamatwa akiwa na  silaha   moja aina ya  gobore huku akiwa  nayo shambani kwake kwa lengo la kuwindia wanyama .
Pia  polisi memkamata  mtu mmoja alijulikana kwa jina la  Donath Laulent  32 Mkazi wa Kijiji cha  Simbesa akiwa na bunduki aina  ya gobore  akiwa ameificha kwa kuifadhi  kwenye majani  nje ya  nyumba yake .
Kaimu kamanda  Rashid Mohamed alisema  jeshi la polisi linaendelea na msako wa kuwatafuta watuhumiwa waliotelekeza pikipiki kwa kumtafuta mmiliki harali wa pikipiki hiyo ili kuweza kuwabaini walikuwa na silaha hizo za kivita .
Ambapo watuhumiwa wawili walioatwa na  gobole bado wanashikiliwa na polisi wanatarajiwa kufikishwa mahakamani  ili wakajibu tuhuma zinazo wakabili .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa