Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Mwaniroma
Nzura (53) Mkazi wa Kijiji cha
Kawanzige Kata ya Kakese Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi umeuwawa kwa kukatwa
na mapanga wakati akiwa ndani ya nyumba yake akiwa amelala na watoto wa mdogo wake
Kwa mujibu wa
Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Kamishina Msaidizi Mwandamizi
Dhahiri Kidavashari tukio hilo lilitokea
tarehe moja june mwaka huu majira ya saa
saba usiku nyumbani kwa marehemu kijijini hapo
Alisema siku hiyo
ya tukio marehemu alikuwa amelala
nyumbani kwake na watoto wawil wa mdogo
wake waitwao Mwajuma
Shururu (4) na Amosi Shururu(3
Alieleza ndipo
wahuaji hao wasio fahamika walipovunja mlango wa nyumba hiyo ya marehemu na mlango huu
uliangukia ndani ya nyumba ambapo iliwafanya waweze kuingia ndani ya nyumba huku
marehemu akiwa amelala usingizi
Kamanda
Kidavashari alisema baada ya wauaji hao wasiofahamika kuingia ndani walianza
kumshambulia marehemu Mwiniromwa kwa mapanga sehemu za kichwani huku watoto wa mdogo wake wakiwa wanashudia
kitendo hicho
Baada ya ya kumshambulia kwa kumkatakata na
mapanga wahuaji hao walipohakisha kuwa
Mwiniromwa ameisha fariki dunia walitokomea
gizinahuku watoto hao
wakiwawaendelea kupiga mayowe ya kuomba msaada kwa majirani ambao walifika kwenye eneo hilo na kumkuta marehemu akiwa ameisha fariki
Dunia
Kamanda
Kidavashari amesema watuhumiwa wa tukio la mauwaja hayo bado hawaja kamatwa na jeshi la polisi
linaendelea na msako wa kuwabaini wauwaji wa mauwaji hayo ya kinyama
Aidha jeshi la
polisi mkoa wa Katavi limetowa wito kwa
wananchi kuendelea kushirikiana na
jeshi la polisi katika kuimarisha ulinzi na usalama katika Mkoa wa Katavi ikiwa na pamoja
na kupinga vitendo vya mauwaji ya kikatili kwa kutowa taarifa kwa jeshi la polisi
Home »
» Auwawa kwa kukatwa na mapanga akiwa amelala ndani ya nyumba yake
0 comments:
Post a Comment