Home » » HALMASHAURI ZATAKIWA KUCHANGIA FEDHA KWA AJIRI YA UNUNUZI WA DAWA ZA HOSPITAL

HALMASHAURI ZATAKIWA KUCHANGIA FEDHA KWA AJIRI YA UNUNUZI WA DAWA ZA HOSPITAL

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Hospitali ya Wilaya ya Mpanda inakabiliwa  na  tatozo la upungufu wa  madawa mbalimbali ya kuwatibia Binadamu kutokana  na  Hospitali  hiyo kutowa  huduma ya  kuwahudumia  wakazi wote wa Mkoa wa Katavi huku Halmashauri  zilizopo  Mkoani hapa  zikiwa zimeshindwa  kuchangia fedha za ununuzi wa dawa  licha ya wakazi wa Halmashauri zao kupatiwa huduma  katika Hospitali hiyo
Haya yalisemwa hapo jana kwenye kikao  cha Baraza la madiwani la  Halmashauri ya  Wilaya ya Mpanda kilichofanyika katika ukumbi wa  Maji  na mganga Mkuu wa Wiliya ya Mpanda Dr Joseph  Msemwa
Dr Msemwa alilieleza  Baraza la Madiwani kuwa Hospitali ya Wilaya ya Mpanda  inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa dawa za Binadamu kutokana   na Hospitali    hiyo  kumiwa na wakazi  wote  wa Halmashauri  za Mkoa huu kupatiwa huduma   na Hospitali hiyo
Aliwaeleza  Madiwani kuwa  licha  ya Halmashauri hizo  wananchi wake kupatiwa huduma  hapo  zimekuwa zikiombwa zichangie  kununua  dawa lakini zimeshindwa kufanya hivyo na matokeo yake mzogo wote wa kuihudumiaHospitali hiyo imeachiwa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda peke yake licha ya kuhudumia Mkoa mzima wa Mkoa wa Katavi
Dr Msemwa alifafanua  kutokana na  kuelemewa  kwa Hospitali hiyo ndio maana walikuwa wameomba  Hospitali hiyo ipandishwe  hadhi na kuwa Hospitali ya Mkoa wa Katavi lakini ilishindikana   kutokana  na kukosa  vigezo
Mganga mkuu huyo wa Wilaya alilazimika kutowa   maelezo hayo kufutia  madiwani wawili Diwani Nassor Kasonso wa Kata ya Kabungu na Thiodela Kisesa wa viti maalumu  kutaka yatolewe maelezo ya kina  kinachosababisha Hospitali hiyo kuwa   na tatizo la upungufu wa dawa za  mara kwa mara
Pia   Diwani Kasonso   aliishauri Halmashauri hiyo kuwa na utaratibu wa kuwafanya  mawakala  wanaofanya shughuli za kukusanya ushuru  wawe wanapewa barua  ya kuwatambulisha  madiwani kwenye eneo usika tofauti na ilivyo sasa ambapo  mawakala wanaokusanya ushuru hata  Diwani wa kata husika wanakuwa hawafamiani
Kwaupande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Justine Tibenderana alikiri kuwepo kwa tatizo la  mawakala kutofahamika kwa madiwani wa kata husika hivyo Halmashauri inaandaa utaratibu wa  kuwa wanawaandikia barua madiwani za kuwatambulisha wakala husika na wakala kabla ya kuanza shughuli  atalazimika kulipoti kwa Diwani wa eneo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa