Home » » WATANZANIA WASHAULIWA KUTEMBELEA HIFADHI ZA TAIFA

WATANZANIA WASHAULIWA KUTEMBELEA HIFADHI ZA TAIFA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399


      Walter  Mguluchuma   Na  Arine  Temu
         Katavi .
Kaimu  Muhifadhi Mkuu  wa  Hifadhi  ya  Taifa  ya  Katavi  Elias  Manase  ametowa  rai kwa Watanzania  wajenge   utamaduni wa kutemmbelea  Hifadhi za  Taifa  kwani  maeneo hayo ni muhimu sana  na waone ni  kama  sehemu  ya maisha yao ya kila siku kwani gharama ya kutembelea Hifadhi ni  ndogo   ukilinganisha  na  gharama ya mtu  anayotumia  kwenye Bar.
Wito  huo  aliutowa  hapo  jana  wakati  alipokuwa  akizungumza na  Wandishi wa  Habari wa  Chama  cha  Wandishi wa  Habari  Mkoa wa  Katavi waliotembelea  Hifadhi ya  Taifa ya  Katavi .
Alisema  pamoja na  Hifadhi   ya  Taifa ya  Katavi  kuwa   na  wanyama   adimu  bado  idadi ya Watalii wa  ndani  na wanje  wanaofika  kutembelea  Hifadhi  hiyo ni  wachache .
Hifadhi  hiyo  ambayo  ni miongoni mwa  Hifadhi  16  zilizopo  hapa  nchini  ni  ya  tatu kwa  ukubwa  ikiwa inazifuatia  Hifadhi za  Ruaha  na   Serengeti .
  Alisema  hifadhi  hiyo  ina  makundi  ya  Wanyama   wengi   adimu  kama  vile  makundi  makubwa ya   viboko  na    Mbwa  mwitu  na    wanyama  wengine    aina ya  kudu  na  maporomoko ya  maji
Alifafanua  kuwa  pamoja  na  kuwepo  na  vivutio  hivyo   idadi ya watalii  bado  halidhishi   ingawa  kunaongezeko  la  watalii   tofauti  na  hapo  awali .
Manase alisema   Hifadhi   ya  Katavi   inakabiliwa  na  changamoto  mbalimbali  zinazoikabili   Hifadhi  hiyo ya  Taifa  ilianzishwa  rasmi   mwaka  1974.
Alizitaja  baadhi ya   changamoto  hizo  kuwa  ni  ujangili  , uingizwaji wa mifugo  ndani ya  Hifadhi na   kupakana  na  kambi za  Wakimbizi  ambapo  watu  wanao ishi kwenye  kambi  hizo  wamekuwa wakiingiza  silaha  kutoka  nchi  jirani  na kufanya  ujangili  ndani ya  Hifadhi .
  Changamoto  nyingine   ni miundo  mbinu ya barabara    pamoja  na uchache wa      Hotel za kulala Watalii   ndani ya  Hifadhi  na  nje ya  Hifadhi .
MWISHO


.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa