Home » » WAKAZI WA KITONGOJI CHA MARADONA WAFARIKI DUNIA BAADA BAADA YA KUNYWA DAWA ZA KIENYEJI

WAKAZI WA KITONGOJI CHA MARADONA WAFARIKI DUNIA BAADA BAADA YA KUNYWA DAWA ZA KIENYEJI

 
 
Na   Walter Mguluchuma.
          Katavi


WAKAZI  watatu  wa  kitongoji cha Senta ya Maradona , kijiji cha
Kabange wilaya mpya ya Tanganyika mkoani Katavi  wamekufa baada ya
kunywa  dawa  ya kienyeji  waliyopewa na  mganga wa kienyeji  aitwae
Msajigwa  Jaheda (55) ili kutibu magonjwa ya tumbo ..

Kamanda  wa Polisi  wa  mkoa  wa Katavi ,  Damas Nyanda amewataja
marehemu hao  kuwa  ni pamoja na Kabula Joseph  (23)  ambao ni  wake
wa mtoto  mdogo  na mtoto  mkubwa wa mganga huyo wa kienyeji ,
mwingine  ni Idulu Masanja (30).

Kamanda Nyanda alieleza kuwa  tukio hilo  lilitokea Oktoba 13 , mwaka
huu  saa nne  usiku  katika kitongoji cha Senta ya Maradona , kijiji
cha Kabange , Kata  ya Sibwesa  katika  wilayani mpya  ya Tanganyika
mkoani humo .

Aliongeza kuwa  mganga  huyo  wa kienyeji  anatafutwa na polisi ambapo
 alitoroka  na kujificha kusikojulikana  baada ya  kutenda uhalifu huo
.

Akisimulia tukio hilo , Kaimu Mganga Mkuu wa Manispaa  ya Mpanda , Dk
Mohamed Mpunja  ambaye  alienda  eneo  hilo  la tukio  alisema kuwa
alisema   usiku huo  wa tukio  mganga  huyo wa kienyeji  alimpatia
mke wa  mtoto  wake mdogo  aitwae Kabula  dawa ya kienyeji ya
kusafisha tumbo .

Aliongeza  kuwa baada  ya kunywa dawa  hiyo, Kabula  alianza kutapika
na kupoteza nguvu mwili  hatimae  akafikwa  na umauti .

“Mganga  huyo  alimpatia  mke  wa mtoto wake  mkubwa , aitwae Ndalo
dawa  ya kienyeji  ya kusafisha  tumbo  mara  baada ya kunywa  alianza
kuharisha  na  hatimae akafriki dunia “ alieleza .

Dk Mpunja  alieleza kuwa  mtu mwingine  aliyepoteza  maisha  ni
Masanja ambae  alifika katika kitongoji hicho  kuhani  msiba ambapo
kabla  ya  kurudi  nyumbani  kwake  alienda kwa mganga wa kienyeji ,
Jaheda  ili aitibiwe  tumbo  la ngiri .

“Mganga  huyo wa kienyeji alimpatia  Masanja  dawa ya kienyeji
ambayo aliinywa  ndipo  akanza kutapika na kuharisha  , alifariki
dunia muda mfupi baadae “ alieleza .

Dk Mpunja  amewataka  wakazi  mkoani  humo  wakihisi  dalili za
ugonjwa  waende kwenye vituo  vya  afya vinavyotoa huduma  kwa
matibabu huku  akiwataka  waganga wa kienyeji  hususani  wa tiba
mbadala  wajisajili .

Mwisho



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa