Thursday, December 24, 2015

MTAARUFU MKUBWA WATOKEA NFRA MPANDA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Mtafaharuku mkubwa  juzi  umetokea  juzi  katika   shirika  la Hifadhi  la chakula cha akiba la Taifa (  NFRA) tawi la  Mpanda  Mkoa wa Katavi  baada ya shirika hilo  kusitisha  huduma ya  utoaji wa  mahindi  kwa wafanyabiashara   wenye vibali  vya kusafirisha mahindi kutoka kwenye tawi la Mpanda kupeleka  Mikoa ya Tabora Simiyu ,Geita na Musoma
Tukio hilo lilitokea hapo juzi baada ya Meneja wa  NFRA wa Tawi la Mpanda  Richald  Ruah  kuwa somea  barua  wafanya biashara hao wenye vibali vya kununua mahindi  kwenye  tawi la Mpanda na badala yake waende  wakanunue kwenye matawi ya Laile na Sumbawanga Mkoani Rukwa  barua yenye kumb \ na \ Fa154\ 201\  01 iliyosainiwa na  Anna  Ngoo kwa niaba ya Afisa  mtendaji wa  Mkuu wa  NRFA.
Wafanyabiashara hao baada ya kusomewa  barua hiyo wote kwa pamoja walipinga kitendo cha shirika hilo  la kuwataka  wakachue  mahindi Mkoani Rukwa badala ya Tawi la Mpanda  na ndipo walipoanza kutowa kauli za kupiga uamuzi huo  .
Mmoja wa wafanyabiashara hao  Peter  Masanja  alieleza kuwa yeye alipewa kibali  cha kununua mahindi kutoka tawi la Mpanda  kupeleka Kanda ya ziwa kwenye Mikoa yenye njaa   hivyo hayuko tayari kwenda kuchukulia mahindi yake Sumbawanga kwani kibali chake  kinamruhusu kununulia mahindi yake Mpanda Katavi .
Costantino  Cosmas  mfanyabiashara kutoka Kaliuwa Mkoa wa Tabora alisema kitendo NFRA kuwasitishia vibali vyao vya kuchukulia mahindi Mpanda watakuwa wamepata hasara kubwa hivyo hayuko  tayari   kutekeleza agizo la barua hiyo.
Alisema yeye alikuwa  ameisha anza kupatia  mahindi yake kwenye  behewa la treni katika sitesheni ya Mpanda na tayari alikuwa amefikisha  nusu ya behewa  na hawezi  kwenda kufuatia mahindi ya kujazia bahewa  lake  kwa kuogopa  kulipia chaji ya kuchelewesha kupakia mzigo kwenye behewa.
 Frolensi Malwa   ambae ni mfanyabiashara wa kutoka Musoma  alieleza kuwa  yeye ameisha lipia kwenya Tawi  hilo la Mpanda  tani 185 za mahindi  kwa bei ya tsh 380 kwa kilogramu moja .
Alisema na wenye maroli ya kusombea  mzigo wake huo ameisha walipa  kupakia mzigo kuanzia Mpanda kwenda Musoma na sio Sumbawanga au Laile  na gharama  ya  kusafirishia mzigo  tofauti na tawi la Mpanda  hana uwezo nao kwani fedha za kununulia mahindi hayo alikopa Benki ipo hatari kwake  hata ya kushindwa kurejesha mkopo huo.
Nae  Maneno  Masanja  alisema hayuko tayari  kufuata agizo la barua hiyo  kwani amekaa zaidi ya wiki mbili  akisubilia foleni ya kupakia mahindi na mpaka sasa ameisha ishiwa hela  na alikuwa anakunywa bia sasa hivi hata uwezo wa kunywa bia hana   analazimika kunywa viroba.
 Alieleza  kuwa NRFA  walipaswa kutowa  taarifa ya kusitisha vibali hivyo mapema  sio kama walivyowafanyizia juzi  ni kitendo kibaya kwa wafanyabiashara hao .
Nae Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima ambae alifika kwenye eneo hilo kuwasikiliza wafanya biashara hao huku akiwa na ulinzi Mkali  wa  Askri Polisi waliokuwa na mabomu ya machozi na silaha za moto kutokana na hari iliyokuwepo hapo .
Mwamlima aliwaeleza wafanyabiashara hao kuwa NRFA imekubali kuendelea  kuwazia wafanya biashara hao mazao ya mahindi kwenye tawi la Mpanda kama ambavyo vibali vyao vinanavyoeleza mpaka hapo vitakapo kwisha  hari ambayo iliwafanya wafabiashara hao waanze kushangilia.
Pia alishauri kuwa ni vizuri  taarifa zinazohusu mabadiliko  yanayofanywa na NRFA  taarifa zake ziwe zinatolewa mapema kuliko  taarifa za  kushitukizwa kama ilivyotokea juzi.

No comments:

Post a Comment