Monday, November 2, 2015

WABUNGE WA MAJIMBO YA KAVUU NA MADIWANI WAKAIDHIWA HATI ZA USHINDI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na  Walter Mguluchuma
Katavi
 Msimamizi wa uchaguzi wa Majimbo ya Katavi na Kavuu Mkoani  hapa ambae pia ni Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Razalo Bene  amewakaidhi  hati za ushindi  wabunge wateule na Madiwani  wa  Majimbo hayo
Msimamizi huyo wa uchaguzi  aliwakaidhi  hati  hizo  hapo  jana  kwa  nyakati  tofauti kwenye  majimbo    majimbo ya Kavuu katika  Tarafa ya Mpimbwe na  Katavi  katika  ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Mlele  huko  Inyonga
Kwa  upande wa  jimbo  la Katavi  msimamizi  huyo  alikadhi  hati ya  ushindi kwa  Mbunge mteule wa Jimbo hilo  Mwandisi  Izack  Kamwelwe(CCM)  na  Madiwani wa  Kata  sita  za Jimbo  hilo
Jimbo  la  Kavuu alikabidhi  hati ya ushindi  kwa  Mbunge  mteule wa jimbo  la Kavuu Dr  Pudensiana Kikwembe (CCM)  pamoja   na  madiwani  tisa wa jimbo hilo
Akizungumza  mara  baada ya  kukabidhiwa    hati   ya  ushindi   Mbunge mteule wa  Jimbo  la  Katavi  Mwandisi    Kamwelwe  alisema  uchaguzi  katika  jimbo  la  Katavi  ulikuwa huru  na  haki
 Alisema   kwenye    jimbo  hilo   taratibu  zilifuatwa  na  ndio  maana   wagombea  wa  jimbo  hilo hawakuweza  kugombana   katika   mchakato  wote  wa uchaguzi   kwenye  jimbo  hilo
 Kazi  iliyopo mbele  yao  viongozi  waliochaguliwa  ni  kuwatumikia wananchi  wote   bila  kujali  itikadi  za   vyama  vya   alisema   Mwandisi  Kamwelwe
Jumla  ya  vyama  vitatu   vya   siasa    vya  CCM, CHADEMA   na ACT  Wazalendo   vilishiriki  uchaguzi  huo    ambapo  Chama  cha  Mapinduzi  kilishinda  ubunge kwenye  majimbo  hayo   na  nafasi  za  udiwani   kwenye  Kata   zote  za   wameshinda  wagombea  wa CCM



    

No comments:

Post a Comment