Friday, October 30, 2015

HOT NEWS: ALIYEGOMBEA UBUNGE NA KUSHINNNDWA (ACT WAZALENDO ) ATAANZA KAMPENI WIKI IJAYO KWA AJILI YA UCHAGUZI WA 2020‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

ALIGOMBEA  UBUNGE(ACT WAZALENDO) KUANZA KEMPENI WIKI IJALO KWA AJIRI YA UCHAGUZI MKUU WA 2020
Na  Walter Mguluchuma
Katavi
Aliyekuwa  mgombea wa Ubunge wa jimbo  la Kavuu la Kavuu Mkoa wa Katavi  katika uchaguzi mkuu wa Oktoa 25 mwaka huu kupitia Chama cha ACT WAZALENDO Stansilaus Kisesa  amehaidi kuanza  kempeni    wiki ijalo  kwa ajiri  ya maandalizi ya  kugombea Ubunge wa Jimbo hilo katika uchaguzi Mkuu wa  mwaka 2020
Kisesa alitowa  kauli hiyo ya kuanza kampeni wiki ijalo wakati alipokuwa akizungumza hapo  jana  na Waandishi wa  Habari hapo jana kwenye hotel ya Victoria  Mjini  hapa
 Alisema kuwa  anatarajia kuanza  kuanza   kampeni  za  kugombea  ubunge wa Jimbo la Kavuu ikiwa  ni maandalizi ya kugombea  tena  kwa   mara ya pili  jimbo  hilo  katika uchaguzi  mkuu ujao  wa  mwaka  2020
 Alifafanua kuwa   katika  uchaguzi wa Oktoba 25 mwaka huu hakuweza kufanya  vizuri   na  ndio  maana  ameamua   kuanza  kampeni  za kugombea jimbo  hilo  mapema
 Alisema  lengo  lake  la  kugombea  ubunge  kwenye  jimbo  hilo  katika uchaguzi  mkuu uliopita  ilikuwa  ni  kutangaza kwanza  jina  lake  na   Chama chake  cha  ACT WAZALENDO kwa ajiri ya  maandalizi ya uchaguzi  mkuu wa   mwaka  2020
Kama jina  langu   na   chama  changu  tayari    tumetangazika  sioni  sababu ya kutoanza  kampeni wiki  ijalo   ili  nijiandae  na    uchaguzi ujao  alisema   Kisesa
Katika  uchaguzi     wa   kugombea ubunge    wa  jimbo hilo  mgombea  ubunge (CCM)  Pudensiana  Kikwembe  alishinda  kwa  kupata kura  18,009 akifuatiwa  na  mgombea  wa  CHADEMA  Laulenti  Mangweshi  aliyepata kura   11,185 na  Stansilaus  Kisesa   ACT WAZALENDO alipata kura  202
Jimbo  hilo  la  Kavuu  katika  uchaguzi wa Oktoba  25 lilikuwa na wagomea wa  nafasi ya  ubunge watatu kutoka  vyama  vya CCM, CHADEMA  na  ACT  Wazalendo

No comments:

Post a Comment