Monday, June 15, 2015

LOWASSA APATA WADHANI 3,450MKOANI KATAVI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma 
Katavi
Waziri  Mkuu   wa  zamani  Edward  Lowasaa  amepata wadhamini  3,450  Mkoani  Katavi  walomdhamini  fomu  za  kugombea  Urais  kupitia  CCM   kwa ajiri ya uchaguzi ujao
 Lowassa  aliwasiri jana   mchana  akitokea  Mkoani  Kigoma  ikiwa ni  mwendelezo  wa ziara  ya kuzungukia  mikoani  kutafuta  wadhamini  wa kumdhamini  ili kugombea  Urais  kupitia  CCM
 Lowassa aliwasiri  uwanja wa  ndege wa Mpanda  majira ya saa  6.33  mchana  ambapo alipokewa na  umati  mkubwa wa  wananchi wa mji wa Mpanda  na mamia ya waendesha pikipiki   ambao waloongoza  msafara na kuelekea  ofisi ya CCM ya  Mkoa wa  Katavi iliyoko  katika  mtaa wa Kasimba huku umati mkubwa wa watu wakiwa wamejipanga pembezoni mwa barabara
 Baada ya  msafara wake huo kutoka  kwenye  ofisi  za  CCM mkoa  ulielekea  kwenye  ofisi za  CCM  Wilaya ya  Mpanda  ambapo  kulikuwa na umati mkubwa wa  watu waliokuwa  na shauku ya kumsikiliza
 Katibu wa  CCM  wa  Wilaya  ya  Mpanda   Elizebeth  Kashili  alieleza kuwa jumla ya wana CCM 3,450 wamejaza fomu za kumdhami ni  Edward  Lowassa
 Alifafanu kuwa  katika  fomu ya kwanza jumla ya wanachama  45 wa CCM wamemdhamini kwenye fomu hiyo na fomu ya pili jumla ya wanachama  3,405 na tano wamemdhami ni  kwenye  fomu  hiyo
Kwa upande wake  Lowassa  aliwashukuru wana CCM  waliojitokeza kwa wingi katika kumdhamini kwenye fomu hizo na aliwashukuru wananchi wa mji wa Mpanda kwa mapokezi  makubwa waliomfanyia ambayo yeye aliyaita ni mapokezi ya aina yake
 Pia  aliwataka wananchi wa Mkoa wa Katavi  waliojiandikisha kwenye  daftari la  kupiga kura  wahakikishe wanavilinda  vitambulisho vyao  kwani ndivyo vitakavyo wasaidia wakati wa kupiga kura na wajiepuke na watu  watakao taka kuwashawishi  kununua vitambulisho vyao
 Hata hivyo haweza kuwaendelea kuwahutubia wananchi hao waliokuwa na shauku ya kumsikiliza  kutokana na kile alichodai kuwa chama kimeisha wakataza wagombea wote kutozungumza  lolote kwa sasa




       

No comments:

Post a Comment