Friday, June 12, 2015

JELA KIFUNGO CHA MIAKA 30 KWA KOSA LA UBAKAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma 
Katavi
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda  Mkoa wa Katavi imemuhukumu  kifungo cha miaka 30  jela    Atanazi    Julias(30)   Mkazi  wa  Mjini  hapa  baada ya kupatikana na  hatia ya kumbaka  kwa nguvu  msichana(23)  mkazi wa mtaa wa  Mji  mwema   mjini  Mpanda
  Atanazi   Juliasi   Mkazi  wa  Mtaa wa Kotazi   Mjini  hapa  alihukumiwa  hukumu  hiyo  jana  mbele  ya   Hakimu   Mkazi  wa   Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Odila  Amworo   baada ya mahakama kulidhika  na ushahidi uliotolewa  Mahakamani  hapo na  mara baada  kutolewa  hukumu hiyo mshitakiwa alianguka na kupoteza fahamu kwa muda
 Awali  katika  kesi hiyo  mwendesha  mashitaka  Mkaguzi  msaidizi wa  Polisi   Godfrey    Ndangala  aliiambia  mahakama kuwa  mshitakiwa huyo  alitenda  kosa  hilo   hapo  januari  30  mwaka huu majira ya saa sita mchana  katika mtaa wa Mji  mwema mjini hapa nyumbani kwao na  msichana aliyebakwa
 Ilidaiwa  Mahakamani  hapo  kuwa siku  hiyo ya  tukio  mshitakiwa  alifika  nyumbani kwao  na  msichana  huyo   na hakuweza kuwakuta wazazi wa  msichana  huyo 
Mwendesha  mashitaka  Ndangala  aliiambia   mahakama  kuwa  mshitakiwa alifika  mida  hiyo nyumbani kwa msichana  huyo baada ya kujua wazazi wake   wote   mida  hiyo huwa wanakuwa  hawapo  nyumbani  wanakuwa kwenye  shughuli zao za biashara
Alisema  baada ya mshitakiwa  kuwa  amefika  nyumbani  hapo   alimwomba msichana huyo  apatie  maji   maji ya kunywa  kwani  anasikia kiu na ndio shida iliyompeleka  hapo
 Alieleza  mshitakiwa  alikubaliwa ombi lake la kupewa   ya kunywa  na ndipo  msichana huyo alipoingia  ndani na kuchukua   maji ya kunywa  na  wakati  akipewa   maji hayo ghafla mshitakiwa  alimshika  msichana huyo na kuanza kumbaka  licha ya mwanamke huyo  kupiga kelele za  kuomba  msaada  mshitakiwa hakujali  na aliendelea kumbaka
Katika  utetezi  wake  mshitakiwa  aliomba   mahakama imwachie huru kwani  hakutenda  kosa hilo  na  pia  imwonee  huruma kwani  umri wake  bado ni  mdogo
Utetezi huo ulipigwa vikali na mwendesha  mashitaka  ambae  alidai kuwa   vitendo  vya  ubakaji vimekuwa  vikiongezeka siku  hadi siku  katika  Mkoa wa Katavi  hivyo ni  vema Mahakama  itatowa  adhabu  kali kwa mshitakiwa  iliiwefundisho kwa watu wengine  wenye  tabia  kama hiyo ya mshitakiwa
Hakimu  Odila  Amworo akisoma  huku  hiyo    aliieleza  kuwa  mahakama  baada ya kusikiliza kesi   hiyo kwa upande  wa mashitaka na utetezi  mahakama imelidhika  na ushahidi uliotolewa wa mpande washita
 Hivyo  Mahakama imemtia  hatiani   mshitakiwa  Atanazi  Julias i  na  imemtia  hatiani kwa kifungu cha  sheria  No 130( 1) a na kifungu  cha  sheria 131(1)  cha kanuni ya adhabu  sura ya 16  marekebisho ya mwaka 2002 hivyo mshitakiwa amekuhumiwa  kutumikia jela kifungo cha miaka 30 jela
Baada ya hakimu kusoma  hukumu  hiyo  mshitakiwa  alianguka ghafla na kupoteza  fahamu  kutona na mshituko wa adhabu hiyo hata hivyo baada ya muda alipata  fahamu na kisha alipelekwa kwenye gereza la Mpanda kwa ajiri ya kutumikia kifungo hicho cha miaka 30

No comments:

Post a Comment