Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Jeshi la
Polisi Mkoa wa Katavi linamshikilia Lugwa Saimoni ((9)
Mkazi wa Kitongoji cha Kungwi
Wilaya ya Mpanda kwa tuhuma za kumuuwa kikatili
Shija Nyango (45)
Mkazi wa kitongoji hicho kwa
kumkatakata na panga katika sehemu mbalimbali za mwili wake baada ya kumnywesha pombe nyingi ya kienyeji
aina ya komoni kupita kiasi
Tukio la mauwaji
ya kikatili ya mtu huyo lilitokea hapo
juzi majira ya saa tano usiku
katia Kitongoji hicho cha Kungwi
kilichopo Wilaya Mpanda
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia jana waandishi wa Habari kuwa siku hiyo ya tukio marehemu
alifiika kwenye klabu
kinachuza pombe ya kienyeji majira ya saa kumi na moja jioni kinachomilikiwa na Renatha
Ngomeni ambae ni shemeji yake na
marehemu huyo kwa lengo la kunywa pombe
Kidavashari
alisema ilipofika majira ya saa moja mtuhumiwa Lugwa Somoni
alifika kwenye kilabu hicho
walipokuwa wakiuza pombe ya kienyeji aina ya komoni huku akiwa na mwenzake mmoja
aliyetambulika kwa jina moja la
Lugwa Mkazi wa Kijiji hicho
Alisema watu hao wawili walijumuika
na marehemu kunywa nae pombe huku wakiwa wanaendelea kumnunulia marehemu
pombe mfululizo hadi majira ya saa tano usiku
Baada ya
kumnywesha pombe marehemu kwa muda mrefu
na watuhumiwa walibaini kuwa
marehemu amelewa hivyo waliaga na kuondoka kwenye kilabu hicho cha pombe kuwa wanakwenda makwao
Kamanda
Kidavashari alieleza watuhumiwa hao
baada ya muda mfupi walirejea kwenye kilabu hicho cha pombe huku wakiwa
wamwshika mapanga mikononi mwao na
kisha waliinza kumshambulia marehemu
ambee walikuta akiwa anaendelea kunywa pombe kwa kumkata
kata katika sehemu mbali mbali za mwili wake huku marehemu akiwa anapiga mayowe ya kuomba msaada
Alisema pamoja na marehemu kuwa anapiga mayowe ya kuomba msaada watu hao
hawakujari na waliendelea kumshambulia
kwa kumkata na mapanga hadi marehemu
alipofariki Dunia na wao walitokomea
Jeshi la
Polisi kwa kushilikiana na wananchi wakitongoji hicho walifanya msako
mkali na kufanikiwa kumkamata
mtuhumiwa Lugwa Saimoni na bado wanaendelea kumshikilia kwa mahojiano zaidi
Kidavashari
aliwaambia waandishi wa Habari kuwa
jeshi la Polisi bado linaendelea na
msako wa kumsaka mtuhumiwa mwingine aliyejulikana kwa jina la Lugwa mkazi wa
Kiitongoji hicho ambae walishilikiana na mtuhumiwa aliyekamatwa kufanya
mauwaji hayo
Mtuhumiwa Lugwa Saimoni
anatarajiwa kufikishwa Mahakamani
mara baada ya uchunguzi utakapo kuwa umekamilika ili ajibu mtuhuma
zinazo mkabili na chanzo cha tukio hilo bado hakijajulikana
No comments:
Post a Comment