watu watano
wakamatwa na bunduki aina ya Gobole na Risasi
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Jeshi la Polisi
Mkoa wa Katavi linawashikilia watu watano wakazi wa Kata ya Ugala Wilaya ya
Mlele Mkoa wa Katavi kwa tuhuma
za kuwakamata katika matukio
matano tofauti wakiwa wanamiliki Bunduki tatu aina ya Gobole na Risasi kumi na
sita bila kuwa na kibali
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia waandishi wa habari hapo jana
kuwa watuhumiwa hao wote watano walikamatwa
katika mida tofauti hapo juzi wakiwa katika Kijiji cha
Ugala Tarafa ya Ndurumo Wilaya ya Mlele
Tukio la kwanza lilitokea majira ya saa
kumi jioni ambapo mtu
aliyefahamika kwa jina la Lazaro
Zakaria (63) Mkazi wa Kijiji hicho alikamatwa akiwa
na Bunduki aina ya Gobole lenye Namba za usajiri NZ 600 ambayo alikuwa akiimiliki bila kuwa na kibali
Tukio la Pili
lilitokea hapo majira ya saa kumi
na mbili jioni mtu mmoja alitambulika
kwa jina la Robarti Kaumba (80) mkazi wa Kijiji cha ugala alikamatwa akiwa nyumbani
kwake na Bunduki moja aina ya
Gobole isiyokuwa na namba na alikuwa akiimiliki kinyume cha sheria
Kidavashari
aliendelea kuwaeleza waandishi wa Habari kuwa tukio la tatu lilitokea
siku hiyo hiyo ya juzi majira ya saa
moja usiku ambapo mtu aliyefahamika kwa
jina la Shabani Mussa (52) Mkazi wa Kijiji cha
Katombola Kata ya Ugala alikamatwa akiwa na Bunduki aina ya Gobole
aliyokuwa akiimiliki bila kuwa na kibali
Alisema katika tukio jingine Benedictor
Simon(52) Mkazi wa Kijiji cha Ugala alikamatwa akiwa nyumbani kwake majira ya saa tano usiku huku akiwa na
Bunduki aina ya Gobole na Risasi 15 ,vipande tisa za nondo vipande vya mti wa mtutu wa bunduki na Baruti aliyokuwa amehifadhi ndani ya chupa
Na
katika tukio jingine lililo tokea siku hiyo majira ya saa saaba usiku Shabani Mussa (52) Mkazi wa Kijiji cha Ugala
alikamatwa akiwa na Risasi moja ya Gobole akiwa anamiliki bila
kibali
Kamanda
Kidavashari alieleza kuwa watuhumiwa hao walikamatwa kufutia msako uliofanywa
na Askari wa Jeshi la Polisi na TANAPA
watuhumiwa hao
wanaendelea kushikiliwa na Polisi
na watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi utakapo kuwa umekamilika
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
No comments:
Post a Comment