Sunday, April 26, 2015

TFDA YATEKETEZA DAWA ZA BINADAMU NA VIPODOZI NA BIDHAA ZA CHAKULA ZAIDI YA MILIONI TANO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Mamlaka  ya  dawa na chakula (TFDA) Kanda ya Nyanda za juu kusini imeteketeza kwa kuchoma moto  dawa  za  binadamu  ambazo  zimepigwa marufu Vipodozi   na bidhaa za chakula ambazo hazina ubora  na hazifai kwa matumizi ya binadamu  zenye thamani ya zaidi ya milioni tano walizozikamata  kufutia msako walioufanya katika Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi
Mkaguzi wa  Kanda  ya nyanda za juu kusini  wa (TFDA)  Paulo  Sonda  aliwaambia waandishi wa habari hapo jana kuwa  dawa hizo walizoziteketeza kwa moto pamoja na bidhaa za chakula na vipodozi   walizoziteketeza  walifanikiwa   kuzikamata katika msako walioufanya kwa siku tatu katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda na Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda
 Alisema  katika msako huo walioufanya kwa kushirikiana na wataalamu wa Afya wa Halmashauri  za Wilaya ya Mpanda  waliweza kubaini bidhaa zilizopigwa  marufuku zikiwa zinauzwa kwenye maduka mbalimbali
 Sonda  alizitaja baadhi  ya  dawa na bidhaa  walizozikamata  na kuzitekekeza kuwa ni  Amodiaquine, Paracetamol vipodozi  vyenye  viambata  vya mecury
Nyingine  alizitaja kuwa ni  bidhaa za  Juice , Biscut  na  Kahawa  ya kutoka Nchi ya Burundi  ambazo hazina ubora  ambazo waliziingiza nchini kwa njia ya panya thamani ya dawa vipodozi  na bidhaa hizo walizoziteketeza zilikuwa na thamani ya milioni tano na laki tisa
 Alisema   dawa  hizo na bidhaa zisizokuwa na ubora zimekuwa na athari  kubwa kwa watumiaji  hivyo  wafanya biashara  wanaowajibu wa kuhakikisha bidhaa wanazoingiza nchini na kuziuza wawe  wanazihakikisha  zinakuwa na ubora unaokubalika
Alifafanua kuwa  watumiaji wa dawa  na bidhaa  kabla ya kununua   mahitaji yao  wawe na utaratibu  wa kuzikagua  kwa kuangalia   alama  zinazokuwa  zimewekwa kama  zinazoonyesha ubora wa bidhaa
 Alitaja changamoto wanayokabiliana nayo TFDA ni tabia inayofanywa na wafanya biashara kuingiza bidhaa kutoka nje  ya nchi kwa kupitia mipaka  isiyo rasmi (njia za panya)
Nae Mfamasia wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda Victor Kabanga  alieleza kuwa  katika kukabiliana na hari hiyo  tayari kuna timu ya wataalamu   katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda inafanya kazi ya kuhakikisha  dawa na bidhaa  ambazo hazina ubora  haziingii  katika Mji wa Mpanda
 Alisema zoezi hilo ni endelevu  hivyo  wafanya biashara wasifikirie kuwa msako huo ulikuwa ni wa muda bali ni zoezi endelevu  litakalo kuwa linafanyika wakati wote
 Kabanga alieleza  pia wataendelea  kutowa elimu  kwa wafanya biashara juu ya  athari  yaa  kuingiza  bidhaa  na   kuwauzia wananchi bidhaa ambazo hazina ubora unaokubalika
Alifafanua kuwa TFDA imeisha towa mamlaka kwa Halmashauri  kutumia wataalamu wake wa afya kufanya ukaguzi wa kubaini  dawa za binadamu  vipodozi na bidhaa  za chakula  ambazo  wafanyabiashara wanaziuza ambazo hazisitahili kuuzwa
Zoezi hilo la  kuteketeza bidhaa hizo zilifanyika katika dampo lililoko  katika  eneo la Minsumilo na kushuhudiwa na wataalamu kutoka TFDA  Kanda ya nyanda za juu kusini na wataalamu wa Afya kutoka Halmashauri za Mji wa Mpanda na Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda pamoja na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali



No comments:

Post a Comment