Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Mtu mmoja Mkazi wa
Mtaa wa Kawajense Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi amekamatwa akiwa na Nyara za Serikali mafuta ya mnyama Kiboko kufutia msako mkali uliofanywa na Askari wa
Jeshi la polisi na TANAPA
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari
alimtaja mtuhumiwa huyo aliyekamatwa na Nyara za Serikali mafuta ya
Kiboko kuwa ni Mashaka George (32) Mtaa
wa Kawajense
Kidavashari
aliwaambia waandishi wa habari kuwa
mtuhumiwa huyo alikamatwa hapo juzi
majira ya saa tisa na nusu alasiri huko
katika Kijiji cha Kisilami Kata ya Ugala Wilaya ya Mlele
Alieleza
mtuhumiwa alikamatwa kufutia taarifa zilizotolewa kutoka kwa Raia wema kwa
Jeshi la Polisi na Askari wa TANAPA kuwa mtuhumiwa George
amekuwa akijihusisha na uwindaji haramu
Baada ya taarifa
hizo zilizotolewa na Raia wema wanaoishi Kijijini hapo polisi kwa kushirikiana na TANAPA walikwenda
kijijini hapo kwa lengo la kufanya
uchunguzi wa tuhuma hizo
Kamanda wa Polisi Kidavashari alisema baada ya kufika kwenye Kijiji hicho Askari Polisi na askari wa TANAPA walifanya
msako wa kumsaka mtuhumiwa na ndipo walipoweza kumkamata huku akiwa na mafuta
ya mnyama Kiboko zaidi ya lita moja na nusu akiwa ameyahifadhi kwenye chupa
Mtuhumiwa anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi na
anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote mara baada ya uchunguzi wa
tukio hilo utakapo kuwa umekamilika
Alifafanua
mafanikio ya kukamatwa kwa
watuhumiwa mbalimbali ambao wamekuwa wakijihusisha na uwindaji haramu katika
Hifadhi ya Taifa ya Katavi na nje ya hifadhi umetokana na ushirikiano mkubwa na mzuri
uliopo kati ya jeshi la polisi
,Askari wa wanyama pori wa TANAPA na raia wema
ambapo wamekuwa wakiendelea kutoa
taarifa za uharifu na kufanikisha katika ukamataji
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
No comments:
Post a Comment