Home » » HII NI HATARI: AKAMATWA NA MTAMBO WA KUTENGENEZEA SILAHA

HII NI HATARI: AKAMATWA NA MTAMBO WA KUTENGENEZEA SILAHA


N a  Walter  Mguluchuma
Katavi
 Jeshi la Polisi  Mkoa wa Katavi linamshikilia mtu mmoja Mkazi wa Kata ya Ugala Tarafa ya Ndurumo Wilaya ya Mlele Mkoani  Katavi  kwa tuhuma za kumkamata akiwa na mtambo wa kutengenea silaha Bunduki aina ya Gobole  
 Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia waandishi wa Habari jana kuwa mtuhumiwa huyo  aliyekamatwa  kuwa ni  Hamisi  Rehani (68) Mkazi wa  Kata ya Ugala Wilaya ya Mlele
 Mtuhumiwa huyo alikamatwa hapo jana majira ya saa  kumi na mbili jioni wakati akiwa ameuhifadhi mtambo huo wa kutengenezea Bunduki aina ya Gobole  ndani ya nyumba yake aliyokuwa akiishi  yeye na familia yake
Kidavashari alisema  mtuhumiwa huyo alikamatwa kufuatia taarifa  zilizokuwa zimetolewa na raia wema kwa jeshi la polisi kuwa mtuhumiwa Hamisi Rehani amekuwa akijihusisha  na utengenezaji wa bunduki aina ya Gobole  bila kuwa na kibali
 Alifafanua baada ya taarifa hizo kulifikia jeshi la Polisi  lilikwenda  kwenye Kata hiyo ya Ugala wakiwa wamefuatana na Askari wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi
 Kidavashari alieleza baada ya Askari hao kuwa wamefika nyumbani kwa mtuhumiwa waliweza kumpekuwa ndani ya nyumba yake na ndipo walipofanikiwa  kumkamata mtuhumiwa akiwa na mtambo wa kutengenezea Bunduki aina ya Gobole
 Alisema uchunguzi wa awali uliofanywa na Askari wa Polisi na Askari wa TANAPA unaonyesha kuwa  mtuhumiwa huyo amekuwa akitumia mtambo huo kwa ajiri ya kuwatengenezea  Bunduki aina ya Gobole wawindaji haramu  ambao wamekuwa wakiwinda wanyama kwenye Hifadhi ya Taifa ya Katavi
 Mtuhumiwa Hamisi Rehani anatarajiwa kufikishwa Mahakamani mara baada ya uchunguzi wa tukio hilo utakapo kuwa umekamilika ili aweze kujibu mashita yanayomkabili

    
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa