Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mwanamke mmoja
aliyefahamika kwa jina la Suzana
Kingi (40) Mkazi wa Kijiji cha
Mwamkuru Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi ameuwawa kwa kukatwa katwa na mapanga shingoni kichwani na mikononi na
watu wasiojulikana
Tukio hilo la
mauwaji ya kinyama yalitokea hapo juzi majira ya saa tisa usiku nyumbani kwa marehemu kijini
hapo alipokuwa akiishi
Kwa mujibu wa
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari siku hiyo ya tukio marehemu alikuwa amelala kwenye nyumba yake akiwa peke yake jirani
na nyumba waliokuwa wakiishi wakwe zake
Maria Kayungiro na Maria
Nsabi wake wa mtoto wake aitwaye
Paul Charles
Alisema wakati Maria Kayungiro
akiwa chumbani kwake amelala alimsikia marehemu akikimbia
toka kwenye nyumba aliyokuwa amelala akielekea kwenye nyumba ya mtoto wake Paulo
Charles huku akipiga
mayowe ya kuomba msaada kuwa anakufa
Marehemu
alifika kwenye nyumba hiyo ya mwanae
na aliweza kusukuma mlango wa nyumba na kufanikiwa kuingia
ndani hadi chumbani huku akiendelea kupiga mayowe ya kuomba msaada
Kidavashari alieleza
wakati huo muuwaji alikuwa akimfuata
kwa nyuma na bahati mbaya mtoto
wake mwenye nyumba hiyo akuwepo
alikuwa amekwenda kwenye harusi kijiji cha jirani ndani ya nyumba alikuwemo Maria
Nsabi
Alisema ndipo muuwaji huyo aliweza kuingia ndani na kuanza kumkatakata marehemu huku akiwa juu ya kitanda cha mwanae wakati akiendelea kutekeleza
mauwaji hayo alikuwa akimmulika
Maria Nsabi kwa tochi
huku akimtishia kuwa akipiga kelele nae atamuuwa kama mama mkwe wake
Kidavashari
alifafanua ilipotimia majira ya saa
kumi usiku Paulo Charles
alirejea nyumbani kwake kutokea harusini
aliingia ndani na kumkuta mkewe Maria
Nsabi akiwa amekaa chini kimya
na ndipo alipomuhoji kulikoni
Kabla
hajamjibu aliangalia kitandani na kumwona mama yake akiwa anavuja damu alipojaribu kumsehesha hakuweza kujibu ndipo
alipoweza gundua kuwa mama yake ameisha uwawa
Kamanda
Kidavashari alisema ndipo Charles alipotoa taarifa kwa majirani
na kwenye uongozi wa Serikali ya jijiji
na kisha kwa jeshi la Polisi
Alisema uchunguzi
wa awali unaonyesha chanzo
cha mauwaji hayo
yanahusishwa na masuala ya
kishirikina na hakuna mtu wala watu
walikamatwa kuhusiana na tukio hilo na
jeshi la polisi kwa kushirikiana na
wananchi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo

No comments:
Post a Comment