Wednesday, July 9, 2014

HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA YAPATA MAKAMU MWENYEKITI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Na  Walter  Mguluchuma   Mpanda  Katavi   Baraza  la  Madiwani  la  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Mpanda   Mkoa  wa  Katavi  limemchagua  Juma   Hawazi  Ibrahimu ambae  ni Diwani wa  Kata  ya  Mwese  kuwa  makamu  mwenyekiti wa Halmashauri  ya  Wilaya ya  Mpanda  kwa kipindi  cha kuanzia  Julai  2014 hadi  June  2015  Huchaguzi huo  wa  kumchagua  Makamu  mwenyekiti  wa  Halmashaurri  hiyo  ulifanyika  hapo  jana    katika  ukumbi  wa  Idara  ya  Maji  ulioko   mjini  hapa  Kikao   hicho  cha  Baraza  la   madiwani  kiliongozwa  na   Mwenyekiti  wa  Halmashauri  hiyo     Yassin  Kibeliti   ambae   pia  ni Diwani  wa  Kata  ya  Mishamo  Katika   uchaguzi huo wa Makamu  Mwenyekiti  wa  Halmashauri  ya  Wilaya  ya Mpanda  nafasi hiyo  ilikuwa  na  mgombea  mmoja   na  alipigiwa  kura   za  siri  Makamu  mwenyekiti  huyo  alichaguliwa  kwa   kupata   kura  13 katika  ya kura  zote  zilizopigwa  ambapo  kura   zilizopigwa  zilikuwa ni 13  na  hakukuwa  na  kura  hata  moja  iliyoharibika   Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Mpanda  inajumla  ya  Madiwani  kumi  wa kuchaguliwa na  waviti  maalumu  watatu  na   Mbunge  mmoja    Baraza  hilo la  Madiwani  pia  liliwachagua  wajumbe  na  wenyeviti  mbalimbali  wa  kamati  watakao  ongoza  kwa  pindi  cha  mwaka  mmoja  cha  kuanzia  julai 2014  hadi  june  2015   mwakani

No comments:

Post a Comment