Monday, July 14, 2014

Halmashari Mpanda kuanzisha jumuia za watumiaji wa maji


Na  Walter  Mguluchuma
Mpanda Katavi
 Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda  Mkoa wa Katavi kupitia Idara yake ya  Maji  imepanga kuanzisha  jumuia  za watumiaji wa maji katika vijiji  mbalimbali vya Halmashauri hiyo
Hayo yalielezwa  hivi  karibuni na  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda  Estomhn Chang’ah  wakati  wa  mkutano  mkuu wa mwaka wa Baraza la  madiwani  wa Halmashauri hiyo uliofanyika kwenye ukumbi wa idara ya maji
 Alisema  Halmashauri hiyo kwa kutumia kitengo cha idara ya maji  imepanga   kuanzisha jumuia  za watumiaji  wa maji katika vijiji mbalimbali
Chang’ah alivitaja  vijiji  hivyo kuwa ni  Igagala, Ngomalusambo, Majalila , Kabungu , Kapalamsenga, Ikaka,  Isenga  Katuma  na Mwese  vijiji hivyo viko kwenye Tarafa  za Karema , Kabungu na Mwese
Alisema uanzishwaji wa jumuia za  watumiaji maji  unatarajiwa  kuanza kufanyika  kipindi cha robo  ya kwanza  ya  mwaka wa  fedha  wa 2014 na 2015  kwa vijiji vya Ngomalusambo  na Karema
Alifafanua  idara ya maji katika Halmashauri hiyo  inakabiliwa na  changamoto  mbambali  ambazo zimesababisha utekelezaji wa shughuli za miradi  kuwa mgumu
Alizitaja baadhi ya changamoto hizo  wananchi  kutotimiza  michango ya ujenzi wa miundombinu  mipya ya maji  inayohitaji  uchangiaji wa asilimia  tano  hasa katika  uchimbaji wa visima virefu na vifupi,wananchi  kuwa na mwamko mdogo wa uchangiaji
Changamoto  nyingine  ni kutopatikana kwa taarifa  sahihi  kutoka  vijijini  juuya  uharibifu  wa miundombinu  ya maji  kutoka kwa wananchi  pamoja na Halmashauri kuletewa fedha kidogo kutoka derikali kuu kwa ajiri ya idara ya maji
Pia  wananchi kuwa na  dhana  potofu  ya kuwa  miradi ya maji  ni mali  ya Serikali  na wao wananchi  hawahusiki  hivyo kutokuwa na mwamko wa uchangiaji pamoja na  wizi wa vipuri  vya visima  vinavyotumia  pampu  za  mikono

No comments:

Post a Comment