Saturday, July 12, 2014

HATARI: MFANYABIASHARA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI JICHONI



 Na Walter  Mguluchuma  Mpanda Katavi,

MFANYABIASHARA mkazi wa kijiji  cha Katuma  wilayani Mpanda  , Juma Luhanga (29) ameuawa  kwa kupingwa risasi  katika jicho  lake la kushoto  na  watu  wawili  wanaosaidkiwa  kuwa  majambazi  akiwa  dukani kwake .

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi , Focus Malengo  amethibitisha   kutokea kwa tukio  hilo lililotokea  Julai 10 mwaka  huu sa tatu na nujsu usiku  kijijini Katumba  maasrufu kwa uchimbaji  wa  dhahabu  wilayani  humo

Akizungumza na mwandishi  wa habari  hizi  kwa njia ya  siku , Kaimu Kamanda huyo  wa Polisi , Malengo , watu  wawili  wamekamatwa wakihusushwa na mauaji hayo  ambapo  wanaendelea kushikiliwa na Polisi  kwa mahojiano  katia Kituo  Kikuu  cha Polisi  kilichopo  mjini Mpanda .

Amewataja  watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Julius Charles Rajab (27)Mtaa wa Kashaulili   na Keimark Emanuel Mwendapole (20)mkazi wa kitingoji cha Mjimwema  mjini Mpanda.

Akisimulia  mkasa huo  Kaimu Kamanda Malengo alieleza kuwa  usiku  wa tukio hilo  maremu  alikuwa  dukani  kwake  akiendelea na  shughuli zake za kibiashara ambapo  watoto  wake watatu  Vitus Luhanga (18) mkulima , Angelina Luhanga (14)  na Leonard Dickson (12) wote  wanasoma  Shule ya Msingi Katuma walikuwa  sebuleni wakiongea .

“Ghafla  mmoja  watuhumiwa hao  alingia  sebuleni  na  kuwaamuru  watoto  hao watatu  kujisalimisha na kukabidhi fedha  …. Ndipo  baba yao  aliposikia  majibishano hayo na  kwenda  sebuleni na  kukabiliana na mtuhumiwa  huyo  ambaye hakuwa na silaha  yeyote  na kufanikiwa  kumtoa  nje ya  nyumba  hiyo  kisha akafunga mlango kwa  ndani ……

Kisha akaenda  dukani  kwake  ili kufunga  dirisha  la duka  hilo “ anaeleza .

Inadaiwa  wakati  akijiandaa kufunga  dirisha la duka  hilo  ndipo mmoja  wa watuhumiwa hao  alipomfyatulia  marehemu  risasi  katika jicho lake la kushoto na  kufa papo hapo .

Kwa mujibu  wa Malengo  watuhumiwa  hao  walifika  eneo  hilo la tukio  wakiwa  wamaevaa  makoti marefu na   nyuso  zao  zikiwa zimefunikwa ili  wasiweze kubainika  baada ya tukio  hilo  waliondoka  wakiwa wamepakizana  kwenye pikipiki  aina ya SunLG ambayo  namba  zake za usajiri  hazikuweza kufahamiaka mara moja .
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

No comments:

Post a Comment