Saturday, June 21, 2014

Kina mama wakosa huduma za kiliki baada ya waume zao kuwakimbia kupima afya

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na  Walter  Mguluchuma
Mpanda Katavi
Akinamama wengi wa Tarafa ya Mwese katika Halmashauri ya Wilaya ya  Mpanda katika Mkoa wa Katavi wanalazimika kujifungulia nyumbani  kufutia kunyimwa huduma kwenye kiliniki  baada ya  kushindwa  kwenda na waume zao  kupimwa afya zao
Hayo  yalielezwa hapo jana  na Diwani  wa viti maalumu  wa   Tarafa  hiyo  Thiodela Kisesa  kwenye kikao  cha Baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo kilichofanyika kwenye ukumbi wa idara ya maji
Diwani Kisesa alisema  akinamama wajawazito wa Tarafa hiyo  wamekuwa wakikosa huduma ya kupimwa maendeleo ya afya zao  pindi waendepo kupima afya zao  kwenye kiriniki   baada ya watowaji  hoduma  kuwakatalia  kuwapatia  huduma za vipimo  mpaka wawe wamekwenda na waume zao
Alisema  wanaume wengi  wamekuwa wakitakiwa  kwenda na wake zao kupima afya zao  na wake zao  ilikuza kubaini  napema  kama mama   mjamzito  anamaambukizi ya VVU ili kuokoa  vifo vya mama na mtoto
Alifafanua baada ya kuwa ya kukosa huduma hiyo  ya kiliniki akinamama wengi wamekuwa wakilazimika  kujifungulia majumbani  kwao  hari ambayo inafanya uhai wa mama na mtoto kuwa mashakani
Kwa upande wake mganga mkuu wa Wilaya ya Mpanda Joseph Msemwa  alilieleza baraza la madiwani kuwa jukumu la kupimwa afya sio la mama peke yake bali ni la mama na baba
Alisema wapo wanaume wanajua kwamba mama akipimwa na akinekana hana maambukizi ya VVU ajua kuwa na yeye pia hana maambukizi jambo ambalo sio sahihi hata kidogo
Alifafanu  kuwa akinama wote ambao ni wajawazito hata kama hawakwenda na waume zao kiriki wanayo haki ya kupatiwa huduma ya vipimo kama kaida bila kujali hata kama akwenda na mume wake

No comments:

Post a Comment