Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
N a Walter
Mguluchuma
Mpanda Katavi
Halmashauri ya
Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi
imekamilisha vitambulisho 710 kwa ajili ya kuwapatia wazee kwa ajiri ya
vitambulisho vya huduma
ya Afya kwa wazee
Hayo yalielezwa hapo jana na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mpanda
Dr Joseph Mkemwa wakati wa kikao cha Baraza la madiwani
wa Halmashauri ya Wilaya ya
Mpanda kilichofanyika kwenye ukumbi wa
Idara ya maji mjini hapa kilichoongozwa
na mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Yassin Kibeliti
Alisema zoezi hilo la kuwapatia wazee
vitambulisho vya afya litakuwa ni
endelevu kwa ajiri ya kuwawezesha wazee
waweze kupata matibabu bure kwenye Hospital vituo vya Afya na kwenye Zahanati
Alifafanua kwa kutambua umuhimu wa wakuwapatia huduma ya
ya matibabu bure wazee msimu ujao
wa mwaka wa fedha wa 2014 na 4015 zimetengwa jumla ya shilingi milioni saba kwa ajiri ya shughuli za
kutengeneza vitambulisho vingine vya huduma ya
afya ya wazee
Alisema mwaka ujao wa fedha wanatarajia kufika
kwenye maeneo mengi zaidi kwa lengo la
kuwaandisha wazee ili waweze kunufaika na utaratibu wa wa kupatatiwa
matibabu bure
Kwa upande wake
Diwani wa Viti maalumu Thiodola
Kisesa alishauri kuwa ni vema
vitambulisho hivyo vikaongezwa kwani idadi ya wazee huongezeka mwaka hadi
mwaka
Nae Diwani wa
Kata ya Mpanda Ndogo Hamad Mapengo
aliomba zoezi la usambazaji wa vitambulisho vinapokuwa vimekamilika viwe vinasambazwa kwa wakati na kwenye
vijiji vyote husika
Alisema kumekuwepo na malalamiko kwa baadhi ya wazee
kulalamikia kucheleweshewa kupatiwa
vitambulisho vyao pindi vinapo kuwa vimekamilika
Mkurugenzi wa Halmashauri Estomihn Chang’ah alisema tatizo la ucheleweshaji wa upatikanaji kwa
wakati vitambulisho hivyo husabishwa na muandaaji ambae amekuwa avitowi
kwa wakati hata hivyo tatizo hilo
litamalizika hivi karibuni
No comments:
Post a Comment