Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Viongozi wa
Halmashauri za Mkoa wa Katavi wametakiwa kuwahamasisha wananchi wao kujiunga na Mfuko wa Bima ya Afya(NHIF )
ili wananchi wao waweze kupata matibabu
kwa bei nafuu
Wito huo
umetolewa hapo leo na Mkuu wa Mkoa wa
Katavi kwenye maadhimisho ya siku ya wadau
wa NHIF na CHFyaliofanyika kwenye
ukumbi wa Katavi Resort katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Katibu
Tawala wa Mkoa wa Katavi Mwandisi
Emanuel Kalobelo
Alisema
umefika wakati sasa wa kila
Halmashauri kuhakikisha inatunga
sheria ya kumtaka kila mwananchi ajiunge
na mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)
Alifafanua wananchi wa Mkoa wa Katavi ambao idadi yao
inafikia jumla ya watu 564000
wanaonufaika na mfuko huo ni watu 66,000 tuu ambao ndio wamejiunga na
mfuko wa NHIF ambao ni sawa na asilimia 12 ya wakazi wote wa Mkoa wa Katavi
Hivyo ni
muhimu kwa kila Halmashauri kuhakikisha
zinawahamasisha wananchi wao wajiunge na mfuko wa Bima ya afya ili
waweze kupatiwa matibabukwa gharama ndogo
pindi wanapokuwa wameugua
Alisema
Halmashauri ziweke ajenda ya kudumu kwenye ratiba yao ya vikao vyao na kuhakikisha kila kikao wanazungumzia na
kujadili namna ya kuhamasisha mfuko huo wa Bima ya Afya kwenye maeneo yao
Alieleza Mfuko huo uweke utaratibu wa kuwaweka watu wenye sifa zinazositahili watumishi
ambao wanakuwa na sifa zinazositahili
kwenye vituo vyao vyote vya kutolea huduma
Alisema wapo baadhi ya watumishi ambao wamekuwa na tabia ya
kuwanyanyasa watu ambao wanatibiwa kwa
kutumia kadi ya Bima ya Afya hivyo wanachama wanaofanyiwa hivyo ni vizuri wawe
wanatowa taarifa mapema ili watumishi
hao waweze kuchukuliwa hatua za kinidhamu
Aidha alikemea
tabia ya baadhi ya wanachama ya kuazimisha kadi zao kwa watu wengine ambao sio
wanachama wa mfuko hivyo tambia hiyo sio
nzuri na iashwe mara moja
Kwa upande wake
Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa Hamis Mdee
alieleza kuwa lengo la kikao hicho cha siku ya wadau
nikukutana na wadau na kujadiliana na kupeana
taatifa za utekelezajiwa
shughuli za mfuko wa Bima ya Afya
kwa kipindi cha mwaka
mzimana kutowa nafasi kwa wanachama kutowa maoni na ushauri
Alisema mfuko huo
mbali ya kutowa matibabu kwa wanachama wake pia inatowa mikopo kwa wanachama
wake na taasisi mbalimbli na hivi
karibuni walitowa mkopo kwa Hospitali ya Wilaya ya Mpanda wa fedha za kununulia
mashine ya Axrey
Mdee alieleza
kuwa lipochangamoto la upungufu wa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma ambapo tatizo hilo linaweza kupungua kwa
kiasi kikubwa endapo kutakuwa na
usimamizi mzuri kwenye vituo vya kutolea huduma
Alifafanua lengo la mfuko wa Bima ya Afya ni kuwa
na wanachama asimilia 30 ya
watanzania wote ifikapo mwakani 2015 kwani kwa sasa wanawachama asilimia 15
Kwa upande wake
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima aalisema atahakikisha ifikiapo hapo mwakani asilimia 100 ya wakazi
wa wilaya ya Mpanda watakuwa wamejiunga na kuwa wanachama wa Mfuko wa Bima ya Afya
No comments:
Post a Comment