Na Walter
Mguluchuma-Katavi yetu Blog
Mpanda Katavi
Jeshi la Polisi
Mkoa wa Katavi wa Mkoa wa Katavi
linamshikilia Vitus Mlengo
(22) Mkazi wa Kijiji cha
Manga Kata ya Kasokola Wilaya ya Mlele
Mkoa wa Katavi kwa tuhuma za kumsababishia kifo mke wake
aitwaye Aghata Izack
(19) baada ya kumpiga akishirikiana na
Faustina Matheo (31 kwa madai
kuwa marehemu mkewe alikuwa ni mvivu
wa kufanya kazi za shambani na nyumbani
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi
Kamishina msaidizi Mwandamizi
Dhahiri Kidavashari alisema chanzo cha kifo cha mwanamke huyo ni ugomvi baina ya wanandoa hao wawili ulitokea
hapo Aprili 25 mwaka
huu majira ya saa sita mchana nyumbani kwao kijijni hapo
Alisema marehemu
ambae alikuwa ni mjamzito siku
iliyofuata aliamka akiwa anajisikia vibaya kutokana na kipigo aliamua
kwenda kwenye zahanati ya Kasokola iliakafanyiwe uchuguzi na kupatiwa
matibabu lakini kabla
ya kufika kwenye Zahanati alipitia kwa mama yake mdogo aitwaye Anastazia Charles na ndipo
alipomweleza kwamba
anajisikia vibaya kutokana
na kipigo alichopigwa na mume
wake aliyeshirikiana na Faustina
Matheo kumpiga yeye
Alifafanua baada ya kupata tiba kwenye zahanati
hiyo wakati anarudi nyumbani
alipitia nyumbani kwa bibi yake aitwaye
Lucia Ramadhani na kumsimulia
kuhusu kupigwa kwake pia
alimweleza kwamba mumewe alimwambia marehemu asirudi
nyumbani bila mboga
hivyo bibi yake alimmpatia mboga
ya kwenda nayo nyumbai kwa mume
wake
Alisema Marehemu alipofika nyumbani mume wake
alimfukuza na hatimae
aliamua kurudi kwa bibi yake na kulala
hapo hadi kesho yake majira ya
asubuhi aliporudi kwa mumewe ambae alikubali kumpokea na wakaendelea kuishi kama kawaida
Alieleza siku ya tarehe 28
majira ya saa mbili usiku marehemu aliandaa chakula cha usiku
lakini alishindwa kula kutokana
na kujisikia vibaya kiafya na matokeo
yake alianza kutapika huku akiwa analalamika kuwa anasikia mwili
unamuuma pamoja na kichwa na ghafla hari ikabadilika na kuwa mbaya
hari ambayo ilimfanya mume wake aombe msaada kwa jirani yake aitwaye
Alfred
Kasonso na walijitahidi
kumpa huduma ya kwanza lakini hari ilizidi kuwa mbaya
Kidavashari
aliesema baada ya kuona hari inazidi
kuwa mbaya walitafuta usafiri wa
pikipiki kwa lengo la kumuwahisha katika
hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa ajiri ya kupatiwa matibabu lakini wakati wakiwa njia kabla ya kufika hospitali
alifariki Dunia
Alisema mume wa
marehemu na Fausti Mathew wanashikiwa na jeshi la polisi kwa
mahojiano zaidi na endapo itabainika
kwamba wao ndio waliohusik
na kifo cha marehemu watafikishwa
kwenye vyombo vya sheria
No comments:
Post a Comment