Friday, April 25, 2014

MAJAMBAZI YAVAMIA KAMBI YA WACHINAMLELE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WATU wanane  wanaosadikiwa kuwa  majambazi  wakiwa na silaha za  jadi, wamevamia  kambi  ya kampuni  ya  Wachina  wanaotengeneza  barabara  ya kiwango cha lami kutoka Mpanda   hadi  Sitalikei, wilayani Mlele na kumjeruhi  mlinzi wa kampuni  hiyo.
Kamanda  wa Polisi  Mkoa  wa Katavi, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Dhahiri Kidavashari, alisema  tukio  hilo  lilitokea  Aprili 22, saa 5 usiku  katika  kambi hiyo iliyopo  Kata ya Magamba.
Alisema watu hao baada ya kufika kwenye  kambi  hiyo walimvamia  mlinzi, Joseph Sarangi na kumshambulia  kwa mapanga  na  marungu  na   kumjeruhi  kwenye paji la uso na  kichwani   na  kufanikiwa kuiba   betri  ya  gari.
Kidavashari alisema muda mfupi baada ya  tukio hilo, askari walipata taarifa na kuanza  kuwafuatilia na kufanikiwa kumtia  mbaroni  mtuhumiwa, Juma   Athumani (23), mkazi  wa Mtaa wa Tambukareli  mjini  hapa.
Alisema polisi wanaendelea kuwatafuta watuhumiwa   wengine saba ambao walishiriki tukio hilo.
 Chanzo:Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment