Home » » Wavuvi wawili wauawa kwa risasi

Wavuvi wawili wauawa kwa risasi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAVUVI wawili wilayani Mlele, Katavi wameuawa  kwa kupigwa  risasi   na askari wa Game Reserve walipokuwa wakivua samaki  ndani ya  Hifadhi  ya Pori la Akiba la Ugala na mwenzao mmoja kujeruhiwa  kwa risasi.
Waliouawa  wametajwa  kuwa ni James  Mauto (21),  mkazi wa Kijiji  cha  Ugala na  January  Marekani  (18), Mkazi wa Kijiji  cha Mtapenda.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa  wa Katavi, Dhahiri Kidavashari, alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea Februari  28, mwaka huu, saa  tisa alasiri  ndani ya Hifadhi ya Pori  la Akiba la Ugala.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa