Na Walter
Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mkuu wa Wilaya ya
Mpanda Paza Mwamlima amempa siku saba
Mwandishi wa ujenzi wa Halmashauri ya
Mji wa Mpanda Albati Kinyando kuhakikisha jengo la Ofisi ya Mtendaji wa
Kata ya Misunkumilo Wilayani hapa
lililojengwa chini ya kiwango kutokana na usimamizi mbovu wa Idara ya
Ujenzi linafanyiwa marekebisho
Mkuu huyo wa
Wilaya ya Mpanda alitowa agizo hilo hapo
juzi wakati wa ziara yake
alipotembelea kata hiyo ya
Misunkumilo kwa lengo la kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo
Mwamlima
alishitushwa na ujenzi wa jengo
hilo ambalo ni jipya lilijengwa na Kampuni ya Kitu Kizima ya Mjini
hapa mara baada ya kuingia ndani ya ofisi hiyo na
kukuta kuta za jengo hilo ambalo ni
jipya kabisa likiwa kuta zake zikiwa
zimepasuka na milango ya jengo ikiwa imepinda na baadhi ya vyumba vikiwa havina mirando
Kabla ya kutowa
agizo hilo kwa Mwandisi wa Ujenzi Mkuu wa Wilaya ambae pia alikuwa
amefuatana
na wataalamu mbalimbali wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda alipokea
taarifa ya ujenzi wa jengo la ofisi hiyo iliyosomwa na Afisa M
tendaji wa Kata hiyo January Kajungilo
Afisa Mtendaji
alieleza kwenye taarifa kuwa jengo ujenzi wa jengo ujenzi wake
megharimu jumla ya shilingi
milioni 28,630,417 kati ya fedha hizo nguvu ya wananchi walichangia NI
Shilingi milioni 4,126,000 na Halmashauri ya Mji wa Mpanda ilitowa
shilingi milioni 24,516,417
Alisema
ujenzi wa jengo hilo ambao ulujengwa na
Kampuni ya Kitu Kizima Contacter ya
mjini Mpanda ulianza kujengwa
mwezi mei 2012 na jengo hilo lilipaswa kukamilika mwezi Novemba mwaka 2012
Alifafanua jengo hilo
ambalo halijaanza kutumika
limekabidhiwa hivi karibuni huku
mkandarasi akiwa amebaki anadai shilingi
526,000 kati ya fedha zote
Kwa upande wake
Mwandisi wa ujenzi Albati Kiyando alimweleza Mkuu wa Wilaya kuwa atatekeleza agizo hilo kwa kushughulikia
marekebisho ya jengo hilo la Afisa Mtebdaji wa kata kwa kulifanyia
marekebisho sehemu zote
zinazostahili kufanyiwa
marekebisho
0 comments:
Post a Comment