Home » » RC KATAVI AOMBA WAKIMBIZI WALIOKO KWENYE MAKAMBI AMBAO HAWAJA PEWA URAI WAONDOLEWE WANADAIWA PIA KUMTII MKUU WA MAKAZI KULIKO RC NA DC.

RC KATAVI AOMBA WAKIMBIZI WALIOKO KWENYE MAKAMBI AMBAO HAWAJA PEWA URAI WAONDOLEWE WANADAIWA PIA KUMTII MKUU WA MAKAZI KULIKO RC NA DC.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


             Na  Walter   Mguluchuma .
                Katavi .
  Mkuu wa   Mkoa  wa  Katavi    Mejagenerali    mstaafu    Raphael   Muhuga   ameiomba   Serikali    kuwaondoka na  kuwapeleke  kwenye    kambi za   Wakimbizi   Raia     wa   Nchi  ya  Burundi  na   Kongo   ambao  wananchi  kwenye   Makazi  ya   Wakimbizi ya   Mishamo na  Katumba    Mkoani   Katavi   ambao   mpaka  sasa hawaja  pata   urai wa  Tanzania .
Muhuga  alitowa   ombi  hilo   hapo   juzi  mbele ya     Naibu Waziri   wa   Ardhi  Nyumba  na    Makazi    Anjelina     Mabula  wakati  alipokuwa    akimsomea  taarifa  ya   Mkoa  wa   Katavi   katika   Ofisi ya  Mkuu wa   Mkoa wa   Katavi .
  Alisema   Mkoa  wa  Katavi  unazo   kambi  mbili  za   wakimbizi   katika   Makazi ya   Wakimbizi ya  Katumba  na   Mishamo   ambapo   wakimbizi    15,0000  hawajapewa   Urai wa   Nchi  hii  huku   asilimia  90  ya  raia  hao waliokuwa  raia wa  Nchi ya  Burundi wakiwa  wamepewa  Urai wa  Tanzania .
Alieleza  kuwa   Raia  hao  wa  Nchi    jirani   kuendelea   kuwepo   kwenye   kambi  hizo    bila  kuondolewa  na  kupelekwa  kwenye    kambi  nyingine  kumekuwa  kukisababisha     hata  wale  waliokuwa   Raia wa   Nchi ya  Burundi  na  kupewa   urai wa  Tanzania  kutotii  maagizo  yanayo   kuwa     yanatolewa   na    Viongozi  wa    Serikali  wa   Mkoa  na  Wilaya .
Alifafanua  kuwa watu  wanaoishi  kwenye   Makambi  hayo  wamekuwa  wakiwatii  zaidi   wakuu  wao  wa    Makazi  ya  Katumba  na   Mishamo  kuliko  yeye   Mkuu  wa   Mkoa  na   wakuu  wa   wilaya    zilizoko  kwenye   kambi hizo    ambazo  ni  Wilaya  ya  Mpanda  na   Wilaya  mpya  ya  Tanganyika .
 Muhuga  alieleza  kuwa  Serikali imewapatia  urai zaidi ya  watu  laki  moja  wanaishi kwenye     makazi   hayo  na   kabla  ya  kupewa  urai  watu  hao   walikuwa  wakihudumiwa  na    shirika   la  wakimbizi  UNHCR  ammbao  sasa  hivi wameacha  kuwahudumia  watu  hao .
Kutona  na  UNHCR  kuwacha kutowa  huduma   kwa  watu  hao      wamekuwa  wakipata   shida   kupata   huduma  muhimu   hivyo   ni   vema   Serikali    ikatangaza   kuyafunga   makambi  hayo  rasmi  ili  watu  hao   wapatiwe   huduma  na    serikali .
Kwani  kwa  sasa     hata  wanapotewa   maelekezo  ya  kufanya   shughuli  za    Maendeleo wamekuwa  hawatii  mpaka  waagizwe  na   Mkuu wao  wa     Makazi si  Mkuu wa  Mkoa  wa   mkuu wa  Wilaya.
Makazi  ya   wakimbizi  za  Mishamo  iliyoko  katika   Wilaya  ya   Tanganyika  na    makazi ya   Katumba   iliyoko  Wilaya  ya  Mpanda   zilianzishwa  mwaka  1972  baada ya kutokea  kwa  vita  Nchini  Burundi
MWISHO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa