Home » » HALMASHAURI ZA SHAULLWA KUNUNUA NYUMBA ZA NHC KWA AJIRI YA WATUMISHI WAKE .

HALMASHAURI ZA SHAULLWA KUNUNUA NYUMBA ZA NHC KWA AJIRI YA WATUMISHI WAKE .

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na  Walter  Mguluchuma .
      Katavi .
  Naibu  Waziri wa  Ardhi  Nyumba  na   Maendeleo ya  Makazi  Anjela  Mabula ametowa  wito kwa  Halmashauri za  Mkoa wa  Katavi  kununua  nyumba za   Shirika  la   Nyumba   la  Taifa  zilizopo  katika   maeneo ya   Halmashauri  zao   ilikupunguza  tatizo  la  nyumba  za   makazi ya  watumishi  wao .
Naibu  Waziri  huyo  alitowa  wito huo  hapo jana  wakati  alipokuwa  akizungumza  na  viongozi   mbalimbali  wa  Serikali   wa   Mkoa  wa   Katavi  kwenye   ofisi ya  Mkuu wa  Mkoa  wa   Katavi  wakati wa  ziara  yake ya  siku  mbili  Mkoani  hapa ya  lengo la kusikiliza  kero  mbalimbali  za  migogoro ya   ardhi   katika  Mkoa wa  Katavi .
  Alisema   shirika  la  Nyumba la  Taifa  limejenga  nyumba  nyingi   katika  Mkoa wa  Katavi  hivyo  ni   vema   Halmashauri za   Mkoa  huo   zikatumia   furusa  hiyo kwa kuzinunua   nyumba  hizo   kwa   ajiri ya  watumishi wao .
 Alieleza  kuwa    shirika  hilo  limeanzisha  mpango  mpya wa   kununua  nyumba za   shirika  hilo   unaoitwa  mpamgaji  mnunuzi   ambao unampa   nafasi   mtu   mwenye  kipato  kidigo  kununua  nyumba  za   NHC.
Katika    mpango  huo   mpangaji   atalipa   asilimia   25  ya   bei ya   thamani ya kununulia  nyumba  na   kisha   atakaa  kwenye   nyumba  hiyo   bure  kwa  kipindi  cha  miezi  mitatu  na   baada  ya   hapo    ataanza  kulipia  kodi ya   nyumba   ambapo   kodi  hiyo   atakayo   kuwa   analipia  ikifikia   thamani ya  bei ya  kuuzia   nyumba   nyumba    hiyo  inakuwa  ni   mali ya    mpangaji  huyo .
 Pia   Anjela  Mabula  aliliagiza   shirika   la  NHC  kufanya   msako   kwenye  vikundi vya   vijana   ambao walipewa   mashine  za  kufyatulia  matofali   na   vikundi  ambavyo   vitabainika   mashine  walizopewa  na   shirika   hilo na   hazifanyi  kazi   basi    vikundi   hivyo   vinya ng-anywe  na  kupewa   vikundi    vingine   vya    vijana .
Pia  aliziagiza  Halmashauri  za   Mkoa  wa   Katavi  kuhakikisha    zinaweka   mipaka  ya   vijiji      kwenye  maeneo  yao  yote   ili  kuepusha   migogoro   ya   ardhi   ambayo  imekuwa  ikitokea  mara  kwa   mara    kutokana  na  kutokuwepo kwa  mipaka.
   Aliziagiza   Halmashauri  za   Mkoa  wa   Katavi   kuhakikisha   zinapima  maeneo ya  mikapa ya  kila  Kijiji  ili  kuondokana  na  migogoro ya   ardhi  na   aliziagiza   zifanye  hivyo  katika  kipindi  kisicho  zidi miezi  mitatu  kuanzia  sasa .
Meneja  wa   NHC    George   Magembe   alisema    shirika   hilo   limejenga   nyumba    95  katika    Mkoa  wa   Katavi   katika   Wilaya   za    Mpanda  na    Mlele .
  Alifafanua   nyumba    70  zimejengwa   katika   Manispaa  ya    Mpanda  katika   eneo  la   Ilembo  na   zimegharimu  kiasi  cha   shilingi  Bilioni   1.1  ambapo   hadi sasa   ni   nyumba     sita  tuu   ambazo   zinawapangaji   huku  nyumba   63  zikiwa   zimekaa  bila  wapangaji     pia  NHC  inajenga  jingo la  kitega  uchumi    katika   eneo la  Paradise    katika  manispaa  hiyo  ya   ghorofa    nne    na  ujenzi wake  utakapo  kamilika  utagharimu  kiasi  cha   shilingi  Bilioni  3.5.
Katika   Halmashauri  ya   Wilaya  ya   Mlele      shirika   hilo   linajenga   nyumba   24  na  wanatarajia   kuanza    ujenzi  wa   mradi   mwingine  wa  kujenga  nyumba   18  za  Walimu  katika   shule ya   Msingi   ya   Kakuni   katika   Halmashauri  ya   Mpimbwe .
MWISHO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa