Home » » HALMASHAURI KUHAKIKI VIKUNDI VYA JINA NA WANAWAKE ILI KUBAINI VIKUNDI HEWA.

HALMASHAURI KUHAKIKI VIKUNDI VYA JINA NA WANAWAKE ILI KUBAINI VIKUNDI HEWA.


       Na  Walter  Mguluchuma .
              Katavi .
   Halmashauri ya   Wilaya  ya   Mpanda   Mkoani  Katavi   inafanya  uhakiki wa  kuvibaini  vikundi   vyote  vya  Vijana  na  Wanawake   kwa lengo la kuvibaini  vikundi  hewa  ambavyo  vimekuwa  vikijipatia mikopo  inayotolewa  na  Halmashauri  hiyo .
  Hayo  yalisemwa  hapo jana  na  Mwenyekiti  wa  Halmashauri ya  Wilaya ya  Mpanda  Hamad  Mapengo  wakati wa kikao cha  Baraza la  Madiwani  wa Halmashauri  hiyo  kilichofanyika   katika  ukumbi wa  Idara ya   Maji .
 Alisema     kumekuwepo  na   tabia  kwenye  Halmashauri  hiyo  kwa  vikundi  vya  Vijana  na  Wanawake vinavyokokeshwa  fedha iliyotengwa kutokana  na  asilimia  tano ya  mapato ya  ndani  kwa  vikundi vichache   kuwa  vina jirudia   kila  mwaka  kupata  mkopo wakati  takwimu zinakuwa zinaonyesha  kuwepo kwa  idadi  kubwa ya    vikundi  huku wanufaika vikiwa ni  vikundi vilevile kila mwaka .
Mapengo  alilieleza  Baraza  hilo  kuwa  kutokana  na   hari  hiyo   ndio  maana  Mkurugenzi  wa  Halmashauri  hiyo  ameanza  kufanya  kazi ya  kuvihakiki  vikundi   vyote   vilivyo  sajiriwa  vya   vijana  na  wanawake  ili  kuvibaini  vikundi  hewa  vyote  vilivyopo  kwenye  Halmashauri  hiyo  watu wasidhani kuwa  Nchi  hii  inawatumishi  hewa tuu  na  mishahara  hewa  bali  pia   hata   vikundi    vipo   ambavyo ni   hewa .
Mwenyekiti  huyo  ambae    ni   Diwani  wa  Kata  ya   Mpanda   Ndogo  aliwaonya  madiwani  wenzake waache  tabia  ya kuvizua   vikundi  kurejesha   fedha  wanazokuwa  wamekopeshwa  na  Halmashauri  hiyo kwa  lengo la  kujitengenezea   siasa   kufanya   hivyo   ni  kuwadanganya  wananchi  wao kwani  fedha  hizo n lazima  zirudishwe  ili  ziendelee  kutolewa kwa  vikundi   vingine .
  Alisema   katika  mwaka huu  wa  fedha  wa  2016  na   2017  Halmashauri   hiyo   tayari  imeisha   tenga  kiasi cha  shilingi  milioni   sabini kwa   ajiri ya kuvikopesha   vikundi  vya   Vijana  na  Wanawake .
Nae  Kaimu   Afisa  Maendeleo  ya  Jamii wa  Halmashauri  ya  Mpanda  Bi   Halma   Kitumba  alilieleza   Baraza  hilo   la  Madiwani  kuwa  wamepanga    kuwakamata    na kuwafikisha  Mahakamani   watu  wote   ambao  walichukua   mikopo  hiyo na  hawajazirejesha  .
Alisema  wameisha  waagiza kuwa  ifikapo  Oktoba   17  vikundi   vyote  viwe  vimerejesha   fedha  walizokopesha  na wale  watakao  shindwa   wataanza kukamatwa  kuanzia   siku  hiyo  ambapo  hadi sasa   tayari wamekusanya  kiasi cha  Tsh 123,000,000.
Mbunge  wa  Jimbo  la  Mpanda   Vijijini  Moshi  Kakoso  alieleza   endapo  fedha  hizo  zinazotolewa  na  Halmashauri  hiyo  na  zitasimamiwa   vizuri  kwenye   vikundi   malengo na dhamira ya   Serikali  itaonekana  katika  mpango wake wa  kuwasaidia   Vijana  na  Wanawake .
Alisema   Madiwani  wanayonafasi  kubwa  ya kuwaelimisha  Wananchi  kwenye  Kata  zao  kuwa  fedha  hizo   zinazotolewa  kwenye  vikundi   sio      fedha  za    sadaka    bali   zitumike  kwa  malengo yaliyokusudiwa na  kisha  kurejeshwa  kwenye  Halmshauri .
 Alifafanua kuwa  makundi  mengi ya   vijana   hayaja kiweke   kwenye   makundi   wanaojiunga  ni  Wanawake  ambao nao  vikundi  hivyo   vimekuwa   haviendelei.
MWISHO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa