Home » » Zaidi ya Wanawake 270 wamefariki Dunia Mkoani Katavi mwaka 2015 kutokana na vifo vilivyo tokana na matatizo ya uzazi

Zaidi ya Wanawake 270 wamefariki Dunia Mkoani Katavi mwaka 2015 kutokana na vifo vilivyo tokana na matatizo ya uzazi




Na  Walter  Mguluchuma .
           Katavi .
Zaidi ya  Wanawake  270   wamefariki   Dunia    Mkoani  Katavi mwaka 2015  kutokana  na  vifo  vilivyo tokana  na  matatizo  ya  uzazi  kwa   kila  vizazi   hai  100,000  idadi  hii  ya  vifo  ni kwa  wale  waliotolewa taarifa   zao.
  Hayo  yalisemwa  hapo jana   na  Kaimu   Mganga  Mkuu  wa  Mkoa wa  Katavi  Dr  Obed  Mahenge  wakati wa  tamasha  kubwa    la Vijana  lililowashirikisha pia wanafunzi wa shule za  Sekondari na chuo cha VETA  Mpanda  tamasha  hilo  ilililoandaliwa  kwa lengo la kutowa elimu     kuhusu  uzazi wa   Mpango  lililoandaliwa  na  Marie  Stopes  Tanzania  kwa  kushirikiana  na  fisi ya   Mganga    Mkuu wa  Mkoa wa  Katavi  lililofanyika  katika  uwanja wa  Shule ya  Msingi  Kashaulili  Manispaa   ya  Mpanda .
 Alisema   katika  Mkoa wa  Katavi  kiwango  cha   vifo   vya  Wanawake   vilivyo tokea  katika kipindi cha  mwaka  jana  kutokana      na  matatizo  ya  uzazi  ni  wanawake 277 kwa  kila   vizazi  hai 100,000 kwa ,idadi   hii  ni  kwa   wale  ambao    taarifa  zao zilitolewa .
Kiwango    cha utumiaji  wa njia  za uzazi wa  mpango   katika  Mkoa wa  Katavi  kwa   mwaka   jana  ilikuwa  ni  asilimia  41.1 tu  kiwango   hiki  kiko   chini   sana  kikilinganishwa  na kiwango  cha   Taifa   cha  asilimia 60.
 
Aidha   imani   potofu  na  taarifa   zisizo  sahihi  kuhusu  uzazi    wa   mpango  zimesababisha   kina   Mama   wengi  kuwa  waoga  wa  kutumia   njia   hizi  na kuishia  kushika  mimba  zisizotarajiwa .
 Alisema  kuwa  Wanawake  wana  haki  ya kutumia  njia ya uzazi wa  mpango  kwa  ajiri ya  afya zao  na   familia  kwa ujumla   hivyo  alitowa  wito kwa  wanaume  wa  Mkoa wa  Katavi  kuwa  bega kwa  bega  na  wake  zao  katika  kutumia   njia  za uzazi wa  mpango  kwani   mwisho  wa  siku   watafaidika  wote  kwa  kuwa  na  familia  yenye  afya  bora .
Mratibu wa  Marie  Stopes  Tanzania wa  Kanda ya  Nyanda  za juu  kusini   Noelia  Mbeyela alisema  wanawake  wengi  hapa  Nchini wamekuwa wakipata  mimba za utotoni huku wakiwa na umri wa chini ya miaka  19 kitu  ambacho ni hatari kwa  afya  zao.
 Alisema  kitendo  hicho  cha  wasichana kupata mimba wakiwa na umri mdogo kimekuwa kikiwasababishia   kupoteza  maisha  yao wakati wa kujifungua  na kupata maambuzi ya VVU  kutokana na kutojua kujikinga   na  maambukizi ya  VVU kwa  ajiri ya kuwa na umri mdogo.
Mbeyela  alieleza  kitendo  hicho  cha kubeba  mimba  wakati wakiwa  bado wadogo kimekuwa    pia kikiwasababishia  kushindwa kuendelea na  masomo kwani  umri huo wa miaka 19 ni  msichana  kuwa   shule  .
Alisema   ushiriki wa  wanaume  kwenye  maswala ya   mpango wa  uzazi  ni   mdogo   sana      swala  hilo  linaonekana   ni  kama  vile  na  wanawake  peke  yao   hivyo  wanaume   wajenge  tabia ya   kufuatana  na  wake  zao  kwenye  maeneo    ambayo   elimu ya  uzazi wa  mpango  inapokuwa  ikitolewa .
Athari  nyingine  ya kuzaa  wakiwa na mri   mdogo  aliitaja  kuwa  ni msichana  kuchukua  jukumu la kuanza kulea  familia  wakati  ajafikia  umri w a  kutunza  familia  matokeo  yake imekuwa ikiathiri uchumi wa  Nchi kwa  Nchi kuwa  na  wategemezi wengi .
Mratibu wa  Marie  Stopes wa  Mkoa wa  Katavi   Seif  Mjuni  alisema   elimu ya uzazi wa  mpango  katika   Mkoa wa  Katavi ilichelewa kuwafikia  wananchi wa  Mkoa huo na  ndio  maana  unakabiliwa na  tatizo  kubwa  la  mimba za  utotoni kwa  wasichana .
 Alisema  wapo watu  wanaamini kuwa   kuzaa   watoto wengi  ni  utajiri  na  wapo  wanaoamini  kuwa  mwanamke ni   chombo cha kuzaa tuu
Aidha  imani potofu  na  taarifa  zisizo  sahihi  kuhusu  uzazi wa  mpango   zimesababisha  kina  mama wengi  kuwa  waoga  wa kutumia  njia  hizi  na kuishia  kushika  mimba  zisizotarajiwa .
Kwa  kutambua  hilo Marie   Stopes  Tanzania  imeanza kutow  elimu ya  afya ya  uzazi wa  mpango  katika   maeneo   yote ya  Halmashauri za  Mkoa wa  Katavi kwa kuwaelisha   faida  za kufuata  uzazi  wa  mpango na kujikinga  na  maambukizi ya  VVU  na  madhara ya  mimba za  utotoni
Nae   Makamu   Meya  wa  Manispaa ya  Mpanda    Kanoni  Lucas alisema  kasi ya ongezeko la watu  Tanzania ni  kubwa  sana   ukilinganisha  na  kasi ya  ukuaji wa  uchumi  wetu  na  hivyo   tusipozaa  watoto  tunao  weza kuwasomesha   tutakuwa tunatengeneza  Taifa  la  watu  dhaifu  katika  ushiriki  wa shughuli za  maendeleo  na  hasa  katika  karne hii  ya  sayansi  na  teknolojia .
 Aliipongeza  Marie   Stopes   Tanzania   pamoja  na  Taasisi   zote  ambazo ni  wadau  katika  kuhamasisha  na kutowa  huduma  za  uzazi wa   mpango  kwa kuonyesha  ushirikiano  kwa  Serikali.
 Alisema  kupitia  Marie   Stopes  Tanzania  na  taasisi  nyingine  huduma  za  uzazi wa  mpango  hususani  huduma  rafiki kwa   vijana   zimepelekwa   karibu  zaidi  na  wananchi   hivyo   afya  za  wananchi   zitaboreka  na  hatimae  kuleta  maendeleo  ya  Mkoa wa  Katavi na   Taifa  kwa  ujumla .
 Katika  tamasha  hilo ambalo lilihudhuliwa na  watu wengi wa lika mbalimbali pia  huduma ya upimaji wa VVU ilitolewa katika   mabanda yaliokuwa yameandaliwa  pamoja na elimu ya uzazi wa  mpango

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa